Print this page

Yanga kushusha majembe mapya

By December 12, 2025 32 0
Kocha wa Yanga, Pedro Goncalves. Kocha wa Yanga, Pedro Goncalves.

DAR ES SALAAM

Na Nicolaus Kilowoko

Kocha mkuu wa klabu ya soka ya Yanga, Pedro Goncalves, amefunguka kuhusu umuhimu wa kufanya usajili, kuelekea katika dirisha dogo la usajili, huku matamanio yake makubwa ni kuwa na kikosi chenye ushindani, katika mashindano ambayo wanashiriki msimu huu.
Goncalves alisema kuwa kufanya usajili ndani ya klabu yake, ni jambo zuri ila ataangalia hasa ni maeneo gani ya kufanya maboresho, kwani tayari ameendelea kuwajumuisha wachezaji wote waliosajili msimu huu, katika mechi mbalimbali.

Rate this item
(0 votes)
Japhet