Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha
Japhet

Japhet

MWANZA

Na Mwandishi wetu

Waziri Mkuu Dk. Mwigulu Nchemba amezitaka Wizara, Mamlaka za Serikali za Mitaa na Tawala za Mikoa, Taasisi na Mashirika ya Umma nchini, kuacha matumizi yasiyo ya lazima ili kuokoa fedha, zitakazoiwezesha Serikali kuendelea kutekeleza miradi ya maendeleo.
Dk. Mwigulu alitaja baadhi ya matumizi yasiyokuwa ya lazima, ikiwemo ununuzi wa magari mapya, wakati yaliyopo yanaweza kuendelea kutoa huduma, kuchapisha kalenda na kununua vifurushi vya zawadi.

ADDIS ABBA,

Ehiopia

Uaskofu Mkuu wa Ethiopia wa Emdibir, umeandaa kikao maalumu cha mafunzo kinacholenga ulinzi wa watoto, mpango unaotajwa kuwa ni muhimu ikizingatiwa kwamba, zaidi ya theluthi moja ya watoto nchini humo kwa sasa, wanakabiliwa na alama kubwa za udhaifu.
Programu hiyo iliundwa kwa ajili ya walimu wa vyama vya watoto katika Parokia mbalimbali, iliyofunguliwa na Mchungaji Abba Tesfa-Amlak Fikre, Mratibu wa Idara ya Uchungaji.

VATICAN CITY,Vatican

Mwadhama Pietro Kardinali Parolin, Katibu Mkuu wa Vatican, ametoa wito kwa Waamini kuona umuhimu wa umoja, kwani umoja katika Kanisa ni zawadi, na kwamba neema si upendeleo bali ni huduma.
Kardinali Parolin aliyasema hayo hivi karibuni, akiwa nchini Denmark kwa siku mbili, kama mjumbe wa Baba Mtakatifu Leo XIV, kwa ajili ya Maadhimisho ya Miaka 1200, ya kuanza kwa utume wa Mtakatifu Ansgar, ambapo alitumia nafasi hiyo pia kuwatia moyo Wakristo, kufanya mazoezi kila wanapopata nafasi

Na  Askofu Mstaafu Method Kilaini

Wahuni:    
Wahuni walikuwa wapiganaji wakali sana, na ndio walioleta matatizo yaliyozusha uvamizi. Wahuni walikuwa watu wa Mashariki ya mbali (Mongoliani, waasia wa ngozi ya njano). Wahuni walikuwa wachungaji wakiishi Kaskazini ya Milima ya Himalaya. 

Malisho yalipoisha, hawa wapanda farasi, walianza kuvamia nchi nyingine. Mwaka 200 Baada ya Kristo (BK), walikwea ukuta wakaivamia China na kusambaratisha himaya yake, na tangu hapo ikawa nyakati za giza kwa miaka 400 iliyofuata kwa China. 

MWANZA

Na Paul Mabuga

Mjadala wa “Uswahili ni nini”, uliibuliwa hivi karibuni na mchambuzi Maggid Mjengwa, akirejea fikra za Jenerali Twaha Ulimwengu na marehemu Edwin Mtei. 
Swali hili limezua taharuki chanya: Je, Mswahili ni nani katika ulimwengu wa leo? Je, bado ni yule “muongo muongo” aliyemchukiza Mtei, au ni utambulisho uliopata sura mpya, kuanzia mitaa ya Dar es Salaam hadi jijini Berlin?
Jenerali Ulimwengu, akizungumza hivi karibuni, katika makiwa ya marehemu Edwin Mtei, alifungua ukurasa wa kumbukumbu uliosisimua wengi. 
Alieleza kuwa Mzee Mtei alikuwa na msimamo usioyumba, dhidi ya kile alichokiita “Uswahili.” Katika muktadha wa kujiuzulu kwake Uwaziri, Mtei aliamini kuwa mfumo wa “Uswahili”, ulikuwa kikwazo kwa uadilifu wa kitaifa.

LONDON, Uingereza
Timu ya soka ya wanawake ya Jersey Bulls, imefanikiwa kuizaba Guildford Saints mabao 30-0, katika mechi ya Ligi ya Soka ya Wanawake ya Kaunti ya Kusini Mashariki mwa Uingereza, maarufu kama Surrey Division One.
Kwa ushindi huo wa maajabu, Bulls imekaribia kufikisha jumla ya mabao 100 ya kufunga, katika mechi zake 11 za Ligi ilizocheza.
Anita Tavares aliongoza kwa mabao tisa, ikiwa ni mara tatu zaidi ya Guildford, ambaye alifunga msimu mzima, huku wachezaji wengine 10 tofauti, wakipata bao katika mchezo huo.

DAR ES SALAAM

Na Arone Mpanduka

Panenka ni mbinu maalumu ya kupiga penati katika mpira wa miguu, ambapo mchezaji hupiga mpira kwa upole na kwa ustadi katikati ya lango, badala ya kupiga kwa nguvu kuelekea pembe za lango. 
Mbinu hii inalenga kumshawishi kipa kwenda upande mmoja, kabla ya mchezaji kupiga mpira polepole katikati, hivyo kumfanya kipa ashindwe kufikia mpira. 

DAR ES SALAAM

Na Mwandishi Wetu

Klabu ya soka ya Singida Black Stars, imesema kwamba ilishindwa kujizuia baada ya ofa nzito kutoka Simba SC, iliyomtaka kiungo mshambuliaji Clatous Chama.
Afisa Habari wa Singida, Hussein Massanza, alisema kuwa mwanzoni hawakuwa na nia ya kumuuza Chama, lakini uongozi wa Simba uliweka mezani pesa nyingi, ambazo ziliwafanya washindwe kumzuia Chama kurejea Msimbazi.

DAR ES SALAAM,

Na Arone Mpanduka

Mchezaji wa zamani wa Taifa Stars, Ally Mayay, amesema kuwa marehemu Peter Manyika amemuachia elimu kubwa ya soka, hasa katika mawasiliano ya uwanjani, wakati mechi ikiwa inaendelea.
Mayay ameyasema hayo wakati akimzungumzia marehemu Manyika (golikipa wa zamani wa Yanga, Mtibwa na Taifa Stars), aliyefariki dunia Januari 26 mwaka huu.

DAR ES SALAAM

Na Mathayo Kijazi

Mkuu wa Idara ya Walei Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Padri Delphinus Ngaiza, amewasihi Viongozi wa Utume wa Wanaume Katoliki (UWAKA) Taifa, kuiga mfano wa Mtakatifu Yosefu kwa kuwa wanyenyekevu, na wenye kumtanguliza Mungu katika mambo yao.
Padri Nagiza alisema hayo hivi karibuni katika homilia yake, wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu, katika Mkutano wa Viongozi hao wa UWAKA, walipokutana kwa lengo la kujadili mambo mbalimbali, yatakayokiendeleza chama hicho cha kitume ngazi ya Taifa, uliofanyika katika Kiwanda cha Woiso Original Products, kilichopo Salasala jijini Dar es Salaam.