Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha
Japhet

Japhet

Mgeta

Na Angela Kibwana

Zaidi ya watoto Wamisionari 300 wa Shirika la Kipapa, Dekania ya Mgeta Jimboni Morogoro, wameshiriki Kongamano la kufunga mwaka, katika dekania hiyo.
Kongamano hilo limefanyika katika Parokia ya Bikira Maria wa Mlima Karmeli-Mgeta, Morogoro, likihusisha watoto kutoka Parokia sita zinazounda Dekania hiyo, kama njia mojawapo ya kuwakuza watoto kiimani na kimaadili, kupitia mafundisho ya semina na michezo mbalimbali.

Dar es Salaam

Na Laura Mwakalunde

Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Sana Jude Thaddaeus Ruwa’ichi, amewataka Waamini kutambua kwamba, Karamu ya Sakramenti Takatifu haikuja ili kushibisha tumbo.
Askofu Ruwa’ichi alisema hayo hivi karibuni, wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya kuzindua Mnara wa Kanisa, iliyofanyika Parokia ya Mwenyeheri Anuarite-Makuburi, jimboni humo.

Morogoro

Na Angela Kibwana

Mhashamu Askofu Lazarus Vitalis Msimbe -SDS, wa Jimbo Katoliki Morogoro, ameongoza Misa Takatifu ya Sherehe ya Bikira Maria Mkingiwa dhambi ya asili, Msimamizi wa Jimbo hilo, na kuwataka Waamini jimboni humo kukimbilia maombezi yake mara kwa mara, ili Jimbo liweze kustawi kiroho na kimaendeleo.
Adhimisho hilo lilifanyika katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Patris, jimboni Morogoro, iliyokwenda sambamba na kufunga mwaka Mtakatifu wa Jubilei ya matumaini miaka 2025, jozi 44 za ndoa Takatifu, pamoja na kutoa shukrani kwa Mungu, kwa mavuno ya Tegemeza Jimbo mwaka huu 2025.

Kisarawe – Pwani

Na Mathayo Kijazi

Chansela wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Padri Vincent Mpwaji, amewaalika Wakristo kutafakari na kutambua kwamba jukumu lao la kwanza la msingi, ni kuwa Mashahidi wa Yesu Kristo.
Padri Mpwaji aliyasema hayo katika homilia yake, wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Sakramenti ya Kipaimara kwa vijana 21, katika Parokia ya Mtakatifu Joseph Cottolengo – Masaki - Kisarawe, jimboni humo.

Dar es Salaam

Na Mathayo Kijazi

Imeelezwa kuwa kila anayepokea Sakramenti Takatifu ya Kipaimara, anatumwa kuwa Mkristo kweli aliye tayari kuacha dhambi na kumrudia Mungu, huku akiwa mtu wa toba.
Hayo yalisemwa na Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Henry Mchamungu, wakati wa homilia yake katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Sakramenti ya Kipaimara kwa vijana 72, katika Parokia ya Mtakatifu Maria Magdalena – Kimara Mtoni, jimboni humo.

LILONGWE, Malawi
Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Lilongwe, nchini Malawi, Mhashamu Vincent Frederick Mwakhwawa, amewataka Waamini kudumisha heshima na uvumilivu wakati wa Misa, akisisitiza kwamba sherehe ya Ekaristi haipaswi kukatizwa kamwe, hata wakati wa changamoto.
Wito huo aliutoa hivi karibuni wakati wa ziara yake ya Kitume, katika Parokia ya Mtakatifu Paulo - Namitete, jimboni humo, ambapo yeye binafsi aliwashukuru na kuwatia moyo washiriki wa Utoto Mtakatifu (Watoto wa Wamisionari).

LILONGWE, Malawi
Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Lilongwe, nchini Malawi, Mhashamu Vincent Frederick Mwakhwawa, amewataka Waamini kudumisha heshima na uvumilivu wakati wa Misa, akisisitiza kwamba sherehe ya Ekaristi haipaswi kukatizwa kamwe, hata wakati wa changamoto.
Wito huo aliutoa hivi karibuni wakati wa ziara yake ya Kitume, katika Parokia ya Mtakatifu Paulo - Namitete, jimboni humo, ambapo yeye binafsi aliwashukuru na kuwatia moyo washiriki wa Utoto Mtakatifu (Watoto wa Wamisionari).

VATICAN CITY, Vatican
Baba Mtakatifu Leo XIV amekutana na kuzungumza na Rais wa Mongolia, Ukhnaagiin Khürelsükh, katika Jumba la Kitume mjini Vatican, ambapo baadaye Rais huyo alikutana pia na Kardinali Pietro Parolin, Katibu Mkuu wa Vatican akiambatana na Monsinyo Mih Blaj, Katibu Msaidizi wa Mahusiano na Mataifa.
Katika majadiliano yao katika Sekretarieti ya Jimbo, Papa na Rais huyo walizungumzia pia uhusiano mzuri kati ya Vatican na Mongolia, kwa nia ya kuuendeleza pia katika nyanja ya kitamaduni.

VATICAN CITY, Vatican

Kiongozi wa Kanisa Katoliki Ulimwenguni, Baba Mtakatifu Leo XIV, amekazia kuhusu furaha ya Mama Kanisa kwa zawadi ya Bikira Maria aliyekingiwa dhambi ya asili, kielelezo cha usafi na utakatifu, ili aweze kumzaa Kristo Yesu, Mwana wa Mungu kwa ajili ya wokovu wa walimwengu, Sherehe ambayo ilitangazwa Desemba 8, 1854 na Papa Pio IX.
Papa aliyasema hayo katika Maadhimisho ya Sherehe ya Bikira Maria Mkingiwa Dhambi ya Asili, kwenye Uwanja wa Kanisa kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican, sherehe ambayo ilitangazwa Desemba 8, 1854 na Papa Pio IX.

VATICAN CITY, Vatican

Mwadhama Pietro Kardinali Parolin, Katibu Mkuu wa Vatican, amefanya hija ya kitume nchini Msumbiji, kama sehemu ya Maadhimisho ya Kumbukizi ya Miaka 30, tangu Vatican ilipoanzisha uhusiano wa Kidiplomasia na Msumbiji, Desemba 14, 1994, miaka 30 iliyopita, sanjari na Jubilei ya Miaka 50 tangu Msumbiji ijipatie uhuru wake wa bendera.
Hayo yalijiri kuanzia Desemba 5 hadi 10, 2025, ambapo tayari Kardinali huyo amekutana na kuzungumza na Viongozi Wakuu wa Serikali ya Msumbiji, wakiongozwa na Rais Margarida Adamugy Talapa.