Print this page

Serena apata kigugumizi kurejea kwenye tenisi

New York, Marekani
Serena Williams anasema kwamba, hana cha kuthibitisha kurudi kwake kwenye tenisi ya ushindani, baada ya kutokuwepo kwa karibu miaka minne, akiongeza kuwa motisha yake kuu, ni matarajio ya binti zake kumuona akicheza tena.
Bingwa huyo mara 23 wa ‘Grand Slam single’, raia wa Marekani alisema kuwa, hakuwa akijiwekea shinikizo lolote anaporudi kwenye mchezo, ambao aliutawala kwa miaka mingi.
Williams alijifungua Olympia, ambaye sasa ana umri wa miaka minane, mnamo 2017, na akarudi kwenye tenisi miezi michache baadaye, na kufikia fainali nne kuu za single, baada ya kupata binti yake mkubwa.
Binti yake wa pili, Adira, alizaliwa mwaka wa 2023, na hajawahi kumuona mama yake akicheza kwenye nyanja hiyo.
Alipoulizwa umuhimu wake wa kuonesha bado anaweza kushinda, Williams alijibu kuwa hahitaji kushinda, kwani ameshinda zaidi ya watu wengi, katika maisha yao yote.
“Kuwa na fursa ya kuweza kufanya hivyo mara ya mwisho, ni jambo la kufurahisha na la kusisimua pia, ni kwamba, kuwa mwanariadha ni jambo bora zaidi, ambalo unaweza kuwa katika nafasi ya juu zaidi”, alisema Serena.

Rate this item
(0 votes)
Japhet