Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam Mhashamu Henry Mchamungu (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Mapadri, WAWATA na Viongozi mbalimbali wa Walei baada ya Askofu kuwaapisha Viongozi wapya wa WAWATA Jimbo sanjari na adhimisho la Misa Takatifu iliyofanyika katika Parokia ya Bikira Maria Mama wa Fatima. Kulia kwa Askofu ni Mlezi wa WAWATA Padri Joseph Mosha na kushoto ni Mkurugenzi wa Walei Jimbo, Padri Vitalis Kassembo.