Print this page

Mashahidi wa Uganda: Watakatifu katika sifa ya kiafrika inayong’ara

Adhimisho la Misa Siku ya Mashahidi wa Uganda. Adhimisho la Misa Siku ya Mashahidi wa Uganda.

Na Dk. Philip Komba

inaadhimishwa ifikapo Juni 3, kila mwaka nchini Uganda, na inakumbusha sadaka ya watu kadhaa, kutoka mahakama ya Mfalme Mwanga II, waliouawa kati ya mwaka 1885 na 1887, kwa kubadili dini na kuwa Wakristo.
Dini hiyo, Mfalme aliiona kama tishio kwa mila za kikabila, na kikwazo cha maisha yake.
Hivyo, kutokana na hilo, Papa Paulo VI mwaka 1969, huko Kampala nchini Uganda, akihutubia Bunge alisema kwamba: “Ninyi Waafrika mnajua maana kubwa ya jumuiya, ni mojawapo ya sifa zenu nzuri na za kibinadamu.”
Kundi la watumishi 22 Wakatoliki (karibu wote ni Waganda), wa mahakama ya Mfalme (Kabaka) Mwanga II wa Buganda, ambao Mama Kanisa aliwatangaza kuwa Watakatifu, waliteswa sana na baadaye kuuawa kishahidi kati ya 1885 na 1887, kwa kutetea imani yao ya kidini.
Watu wengine 150 walikufa katika mapigano kati ya vikundi tofauti, vilivyohusishwa na ushawishi wa wamisionari Wakatoliki au Waprotestanti, na wafanyabiashara wa Kiswahili au Wamisri.
Kifo cha kwanza cha shahidi mnamo Januari 1885, kilifuatiwa mnamo Oktoba, na kile cha Askofu wa Kiingereza J. Hannington na Joseph Mukasa Balikuddembe. Kundi la Waislamu lilimshawishi Mwanga, kuhusu kuhusika kwa Wakristo katika kuchomwa moto, kwa eneo la kifalme (1886), na kwa hiyo ukatili wa mfululizo mpya wa mauaji, uliwashtua sana viongozi wasio Wakristo, kiasi kwamba walizuia mauaji zaidi na hata kusababisha ongezeko la ubatizo. Mashahidi 22 Wakatoliki, walitangazwa kuwa Watakatifu mnamo 1964 na Papa Paulo XIV, ambaye pia alifanya ziara ya Kitume nchini Uganda.
Mtakatifu Paulo VI, alitimiza ziara hiyo kuanzia tarehe 13 Julai hadi tarehe 2 Agosti 1969.  Ziara hiyo ya Uganda mara nyingi, imekumbukwa kwa kutia moyo Kanisa changa la Afrika, kukua katika ukomavu, kwa ajili ya kukuza ubinadamu na kwa ajili ya kutafuta amani.
Papa Mtakatifu akikutana na baadhi ya Waamini wa Kiislamu, katika Ubalozi wa Vatican mjini Kampala alieleza kuwa:
“Tuna uhakika wa kuwa katika ushirika nanyi, tunapomwomba Mwenyezi Mungu, aamshe mioyoni mwa Waamini wote barani Afrika, hamu ya upatanisho na msamaha, ambayo mara nyingi hupendekezwa katika Injili na Kurani.
Na tunawezaje kushindwa kuhusisha na ushuhuda wa uchamungu, na uaminifu wa mashahidi Wakatoliki na Waprotestanti, kumbukumbu ya wale wanaoungama imani ya Kiislamu, ambao historia yao inatukumbusha kwamba, walikuwa wa kwanza mnamo 1848, kulipa kwa maisha yao kwa kukataa kukiuka maagizo ya dini yao?”
Hotuba ya Papa Paulo XIV kwa Uganda
Ndugu msikilizaji na msomaji, vilevile Mtakatifu Paulo VI akikutana na Rais, Mamlaka za kiraia na kikosi cha Kidiplomasia cha Uganda, katika Ukumbi wa Bunge huko Kampala tarehe 1 Agosti 1969, wakati wa hija yake ya kitume alitoa hotuba yake.
Katika muktadha huu wa maadhimisho ya Mashahidi, tunapenda kukumbusha hotuba hii ya Kinabii, katika ziara yake ya kwanza barani Afrika. Maono yake na utabiri wake, ulikuwa kama wa watangulizi wake, na wale ambao walifuata hadi leo hii. Mapapa wote kilio ni kimoja. Katika ulimwengu uliogawanyika vipande vipande na vita, unahitaji amani, haki na usawa.

Rate this item
(0 votes)
Japhet

Latest from Japhet