Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha
Makala

Makala (61)

Mwanza

Na Paul Mabuga

Maandishi yaliyoandikwa kwenye bajaji zetu, ambayo  kwa  muhtasari na kwa  muktadha wa yaliyokusanywa katika makala haya, unaweza kusema ni kama kutoka, “Enzi za Mwalimu” hadi “Kwenye Ndoa Yenu...”:, na vilevile ni maneno yanayosema mengi yenye kusisimua, kuibua hisia, kufurahisha na hata kufikirisha, sembuse kutia hofu na kuogofya.

Ni kwamba licha ya barabara za miji yetu hapa nchini, kujaa watu na shamrashamra za kelele za honi, lakini  pia zimesheheni  falsafa ya Mswahili.. Sio kwenye vitabu au kwenye mikutano ya hadhara, bali kwenye mabango madogo yaliyobandikwa, au kuandikwa nyuma ya magari yetu ya usafiri, na vyombo vingine maarufu kama Bajaji.

Dar es Salaam

Na Pd. Richard Mjigwa- C.PP.S

Ilikuwa ni Novemba 8, mwaka 1984, Mtakatifu Yohane Paulo II (Papa), alipochapisha Waraka unaojulikana kama “Tot tantaeque” yaani “Bikira Maria ameidhinishwa kuwa Mlinzi na Mwombezi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania”, Sherehe inayoadhimishwa kitaifa kila mwaka ifikapo Desemba 9.
Katika mkesha wa uhuru wa Tanganyika, Mtakatifu Yohane XXIII, alitunga Sala Maalumu kwa ajili ya kuiombea Tanganyika, ili uhuru wake uweze kuwanufaisha watu wake.

DAR ES SALAAM

Na Edvesta Tarimo

Afya ya akili ni moja ya vipengele muhimu zaidi vya ustawi wa binadamu, lakini mara nyingi hupewa nafasi ndogo katika mjadala wa afya. 
Hata hivyo utafiti unaonesha kwamba, afya ya akili inajumuisha hali ya kiakili, kihisia na kijamii ya mtu, na ni msingi wa jinsi anavyokabiliana na changamoto za kila siku. 
Licha ya kwamba kila mtu anapitia magumu maishani, kuna njia za kujikinga dhidi ya athari za majeraha ya kihisia (kiwewe), na kujenga uthabiti wa kukabiliana na hali ngumu.

DAR ES SALAAM

Na Shemasi George Timalias

Karibu ndugu msikilizaji wa Radio Vatican, katika tafakari hii, inayotugusa kwa karibu sana, ambayo inakumbusha Sikukuu ya Watakatifu wote, kila ifikapo tarehe Mosi Novemba ya kila mwaka, lakini pamoja na Watakatifu, kuna ndugu zetu Marehemu wote waliotutangulia mbele ya haki, ambapo Mama Kanisa anatupatia fursa ya kuwakumbuka, kila ifikapo  tarehe 2 ya mwezi Novemba na kuendelea hadi mwisho wa mwezi.
Kwa hiyo tuanze tafakari hii, sehemu ya kwanza ya Watakatifu. Fundisho kuu tunalopata katika siku hii ya watakatifu wote, ni msisitizo wa maisha yetu kuishia mikononi mwa Mungu aliyetuumba huko mbinguni.

Katika safu hii ya Chimba Chimba Historia ya Kanisa wiki iliyopita, tuliendelea kuwaletea historia ya kuibuka kwa Dola ya Kikristo, hususani tuliwajuza kuhusu Faida na Hasara za Dola ya Kikristo. Leo tunawaletea historia ya Miundombinu ya Kanisa kuanzia Karne ya nne na tano. Sasa endelea…

Watumishi wa Kanisa na Mitaguso:
Bwana wetu Yesu Kristo, aliacha amewachagua na kuwaweka mitume 12 na wafuasi 70 (72), ili waendeleze kazi aliyoianza (Lk. 6:13-16; 10:1-12). Hawa walirithiwa kama Maaskofu na Mapadri.
Katika Kanisa la mwanzo, polepole kufuatana na mahitaji katika misingi aliyoiweka Kristo, miundombinu hiyo iliongezeka na kuboreshwa.
Kuanzia Karne ya nne na tano, palikuwepo na madaraja saba katika watumishi wa Kanisa. Kati ya madaraja hayo, madogo ni manne yakiwemo Mfungua Mlango, Msomaji, Mtoa Mashetani na Mtumishi wa Ibada, na madaraja makubwa ni matatu, Ushemasi, Upadri na Uaskofu.

Moshi

Na Paul Charles Mabuga

Wiki moja tu inatosha kunasa moyo wako, katika mtego mtamu wa pilikapilika za Moshi. Huu si mji wa kawaida, bali ni lulu iliyolala katika kivuli kitukufu cha Mlima Kilimanjaro.
Huku ukiahidi utulivu wa kitalii, uhalisia wake umejaa mizunguko ya kusisimua, milio isiyotarajiwa, na siri za kitabibu zinazofichwa kwenye glasi ya maziwa ya ngamia, na kikombe cha kahawa bora kabisa duniani.
Nilipowasili, hali ya hewa ilinikumbatia kwa ubaridi laini wa majira haya, ule unaochochea hamu ya kahawa ya moto hata mchana. Lakini ghafla, palikuwa na mabadiliko ya joto! Joto jipya lilianza kuhisiwa ghafla, kana kwamba Mlima Kilimanjaro ulikuwa umeamua kuachia pumzi yake ya joto badala ya baridi. Mabadiliko haya ya ghafla yananukia mabadiliko ya tabianchi, yanayobadilisha mood ya mji.

Dar es Salaam

Na Pd. Gaston George Mkude

Kristo amefufuka kwelikweli, Aleluia, Aleluia!
Somo la Injili Takatifu ya leo imegawanyika katika sehemu kuu mbili. Kwanza ni Yesu anawavuvia Roho Mtakatifu wafuasi wake, na hivyo kuwapa uwezo dhidi ya uovu na yule mwovu, na ndio kuwaondolea watu dhambi zao. Hivyo Pasaka ni sherehe ya kuonja upendo na huruma ya Mungu, na ndio leo Mama Kanisa anatualika katika Dominika hii ya pili ya Pasaka kutafakari Huruma ya Mungu kwetu. Sehemu ya pili ni ile ya mtume asiyeamini bila kuona na kugusa madonda yake Yesu, ndiye Tomaso aliyejulikana pia kama Pacha.
Kabla ya mateso, kifo na ufufuko wake, Bwana wetu Yesu Kristo anawafundisha wanafunzi wake kuwa Yeye ndio Uzima na Ufufuo. Hivyo baada ya ufufuko wake anapowatokea wanafunzi wake siku ile ya kwanza ya Juma anawadhihirishia waziwazi mitume wake kuwa kweli ni mzima, na kuwasalimu kwa kuwatakia amani nafsini mwao baada ya kujawa na hofu na mahangaiko mengi baada ya kushuhudia mateso na kifo cha Bwana na Mwalimu wao. Ni kweli yeye mzima, amefufuka na mauti hayana tena nguvu dhidi yake! Ufufuko ni ushindi dhidi ya mauti na dhambi, ni ushindi wa upendo na huruma ya Mungu dhidi ya uovu na muovu. Pasaka ni tangazo la upendo na huruma ya Mungu kwa ulimwengu mzima. Pasaka ni Habari Njema kwetu tunaokimbilia huruma na upendo wa Mungu!

Na Paul Mabuga

Jua la adhuhuri liliwaka eneo kuu la biashara na lenye shughuli nyingi katikati ya Jiji la Mwanza. Nilimpa muuza magazeti, makala ya toleo la gazeti moja la kila siku la Kiswahili, kwa mwaliko wa kimya kimya wa kumshirikisha kwa habari zinazovutia siku hiyo.
Dakika zilipita, kisha nikauliza: “Ni nini kinakuvutia?” Alionesha tangazo la EWURA, mwanga wa matumaini mbele ya matatizo ya maji yasiyoisha.
“Ni kuhusu suluhisho,” alisema.  Nilisubiri zaidi, lakini kurasa alizipita na baadaye anasema hakuna cha ziada.
Baadaye, kwenye vurugu za soko la Mlango Mmoja. Muuzaji, macho yakimtoka, alilishika gazeti kana kwamba lilikuwa adimu, lakini kumbe kwake ni la gharama kubwa. “Shilingi 1000?” alisema kwa mshangao.
“Hiyo ni chakula cha mchana cha ugali na fulu!” Gharama, sio maudhui, pengine ndio ingeuwa kichwa cha habari kwake kuliko yaliyomo kwenye gazeti.
Kisha katika safari ya kurejea maskani nikiwa nimebanwa kwenye daladala, mazungumzo na jirani yangu, kijana aliyejitambulisha kuwa msomi, yalifunua mtazamo tofauti.
 “Mitandao ya kijamii,” alisema kwa dharau, akipitia kurasa. “Matukio ya moja kwa moja kwenye TV tunaona yote kwa haraka zaidi.” Kwa hiyo Gazeti, mikononi mwake, lilionekana kama halina cha maana, maana mengi alishayapata kabla. ZAIDI KWENYE TUMAINI LETU.

Na Joseph Mihangwa

Katika mkutano wa nchi tajiri duniani (G.8), uliofanyika Gleneagles, mwaka 2005, chini ya kauli mbiu ya “Ufanye Umaskini Uwe Historia”, nchi hizo ziliahidi kuipatia Afrika  dola za Kimarekani bilioni 50 ili zijikwamue kutoka kwenye umaskini.

Mpaka sasa nchi hizo hazijatekeleza ahadi yake, badala yake Afrika inaendelea kupata fedha za mzunguko wa mikopo kwa  masharti magumu.

Masharti hayo ni pamoja na kuuza/kubinafsisha Rasilimali za Taifa, kama tulivyofanya kwa Mashirika muhimu kama Benki ya NBC, NMB na mashinikizo mengine, kama vile kuruhusu vituo vya kijeshi vya Marekani nchini [AFRICOM], kutunga sheria dhidi ya “Ugaidi”, ambacho hiki kinachoitwa “Ugaidi” kusema kweli ni harakati za wanyonge dhidi ya ubabe, ubeberu na ukoloni mamboleo wa nchi za Magharibi.

Si hivyo tu, hata ahadi na misaada inayotolewa siku zote ni chini ya kiwango/kiasi kinachotamkwa. Na kwa mujibu wa taarifa ya Shirika  moja lisilo la Kiserikali barani Ulaya, CONCORD, iliyopewa jina, “Hold the Applause” [Usishangilie], ni kwamba, zaidi ya asilimia 30 ya sehemu ya misaada inayotolewa au kuahidiwa na nchi fadhili, si misaada halisi bali ni misaada iliyobinywa na urejeshaji kubebwa na Serikali inayofadhiliwa. INAENDELEA KWENYE GAZETI TUMAINI LETU.

HISTORIA YA KANISA

Na Askofu Mstaafu Method Kilaini

Mitume na wafuasi wa Kristo toka mwanzo kilele na kitovu cha Imani yao kilikuwa kifo na ufufuko wa Bwana wetu Yesu Kristo. Injili zote zinasimulia juu ya wiki ya mwisho ya maisha ya Bwana wetu Yesu Kristo ulimenguni au kwa naneno mengine tunachoadhimisha kama Juma Kuu ikiwa ni matukio ya  kuwaaga mitume, kushikwa, kufa na kufufuka kwa Bwana wetu Yesu Kristo.
Hiki ndicho kilikuwa kilele cha simulizi zote. Kwa namna ya pekee tunayakuta katika Injili ya Mt. Yohana sura ya 12 hadi 20, ambayo inasimulia kwa kinaganaga juma hilo kuu. Mtakatifu Yohana alikuwa shuhuha wa matukio haya yote na hadi kifo chake aliyakumbuka kwa uwazi, yalimwachia alama kubwa katika maisha yake.
Yesu Kristo alikufa na kufufuka wakati wa maadhimisho ya Pasaka ya Wayahudi. Katika siku hizo Wayahudi humkumbuka Musa na kukombolewa kwao kutoka utumwani Misri. Huadhimisha mapatano kati ya Mungu na taifa lao la  Israel.
Pasaka, yalikuwa ni maadhimisho ya juma zima, wakikumbuka na kusimilia historia yao kuanzia baba zao walipokula chakula cha mwisho huko Misri, ikiwa ni mkate bila kutiwa chachu na mboga chungu na nyama ya kondoo, ambaye damu yake  waliipaka milango yao.

SOMA ZAIDI KATIKA TUMAINI LETU.

Page 1 of 5