Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha
Makala

Makala (55)

Dar es Salaam

Na Pd. Gaston George Mkude

Kristo amefufuka kwelikweli, Aleluia, Aleluia!
Somo la Injili Takatifu ya leo imegawanyika katika sehemu kuu mbili. Kwanza ni Yesu anawavuvia Roho Mtakatifu wafuasi wake, na hivyo kuwapa uwezo dhidi ya uovu na yule mwovu, na ndio kuwaondolea watu dhambi zao. Hivyo Pasaka ni sherehe ya kuonja upendo na huruma ya Mungu, na ndio leo Mama Kanisa anatualika katika Dominika hii ya pili ya Pasaka kutafakari Huruma ya Mungu kwetu. Sehemu ya pili ni ile ya mtume asiyeamini bila kuona na kugusa madonda yake Yesu, ndiye Tomaso aliyejulikana pia kama Pacha.
Kabla ya mateso, kifo na ufufuko wake, Bwana wetu Yesu Kristo anawafundisha wanafunzi wake kuwa Yeye ndio Uzima na Ufufuo. Hivyo baada ya ufufuko wake anapowatokea wanafunzi wake siku ile ya kwanza ya Juma anawadhihirishia waziwazi mitume wake kuwa kweli ni mzima, na kuwasalimu kwa kuwatakia amani nafsini mwao baada ya kujawa na hofu na mahangaiko mengi baada ya kushuhudia mateso na kifo cha Bwana na Mwalimu wao. Ni kweli yeye mzima, amefufuka na mauti hayana tena nguvu dhidi yake! Ufufuko ni ushindi dhidi ya mauti na dhambi, ni ushindi wa upendo na huruma ya Mungu dhidi ya uovu na muovu. Pasaka ni tangazo la upendo na huruma ya Mungu kwa ulimwengu mzima. Pasaka ni Habari Njema kwetu tunaokimbilia huruma na upendo wa Mungu!

Na Paul Mabuga

Jua la adhuhuri liliwaka eneo kuu la biashara na lenye shughuli nyingi katikati ya Jiji la Mwanza. Nilimpa muuza magazeti, makala ya toleo la gazeti moja la kila siku la Kiswahili, kwa mwaliko wa kimya kimya wa kumshirikisha kwa habari zinazovutia siku hiyo.
Dakika zilipita, kisha nikauliza: “Ni nini kinakuvutia?” Alionesha tangazo la EWURA, mwanga wa matumaini mbele ya matatizo ya maji yasiyoisha.
“Ni kuhusu suluhisho,” alisema.  Nilisubiri zaidi, lakini kurasa alizipita na baadaye anasema hakuna cha ziada.
Baadaye, kwenye vurugu za soko la Mlango Mmoja. Muuzaji, macho yakimtoka, alilishika gazeti kana kwamba lilikuwa adimu, lakini kumbe kwake ni la gharama kubwa. “Shilingi 1000?” alisema kwa mshangao.
“Hiyo ni chakula cha mchana cha ugali na fulu!” Gharama, sio maudhui, pengine ndio ingeuwa kichwa cha habari kwake kuliko yaliyomo kwenye gazeti.
Kisha katika safari ya kurejea maskani nikiwa nimebanwa kwenye daladala, mazungumzo na jirani yangu, kijana aliyejitambulisha kuwa msomi, yalifunua mtazamo tofauti.
 “Mitandao ya kijamii,” alisema kwa dharau, akipitia kurasa. “Matukio ya moja kwa moja kwenye TV tunaona yote kwa haraka zaidi.” Kwa hiyo Gazeti, mikononi mwake, lilionekana kama halina cha maana, maana mengi alishayapata kabla. ZAIDI KWENYE TUMAINI LETU.

Na Joseph Mihangwa

Katika mkutano wa nchi tajiri duniani (G.8), uliofanyika Gleneagles, mwaka 2005, chini ya kauli mbiu ya “Ufanye Umaskini Uwe Historia”, nchi hizo ziliahidi kuipatia Afrika  dola za Kimarekani bilioni 50 ili zijikwamue kutoka kwenye umaskini.

Mpaka sasa nchi hizo hazijatekeleza ahadi yake, badala yake Afrika inaendelea kupata fedha za mzunguko wa mikopo kwa  masharti magumu.

Masharti hayo ni pamoja na kuuza/kubinafsisha Rasilimali za Taifa, kama tulivyofanya kwa Mashirika muhimu kama Benki ya NBC, NMB na mashinikizo mengine, kama vile kuruhusu vituo vya kijeshi vya Marekani nchini [AFRICOM], kutunga sheria dhidi ya “Ugaidi”, ambacho hiki kinachoitwa “Ugaidi” kusema kweli ni harakati za wanyonge dhidi ya ubabe, ubeberu na ukoloni mamboleo wa nchi za Magharibi.

Si hivyo tu, hata ahadi na misaada inayotolewa siku zote ni chini ya kiwango/kiasi kinachotamkwa. Na kwa mujibu wa taarifa ya Shirika  moja lisilo la Kiserikali barani Ulaya, CONCORD, iliyopewa jina, “Hold the Applause” [Usishangilie], ni kwamba, zaidi ya asilimia 30 ya sehemu ya misaada inayotolewa au kuahidiwa na nchi fadhili, si misaada halisi bali ni misaada iliyobinywa na urejeshaji kubebwa na Serikali inayofadhiliwa. INAENDELEA KWENYE GAZETI TUMAINI LETU.

HISTORIA YA KANISA

Na Askofu Mstaafu Method Kilaini

Mitume na wafuasi wa Kristo toka mwanzo kilele na kitovu cha Imani yao kilikuwa kifo na ufufuko wa Bwana wetu Yesu Kristo. Injili zote zinasimulia juu ya wiki ya mwisho ya maisha ya Bwana wetu Yesu Kristo ulimenguni au kwa naneno mengine tunachoadhimisha kama Juma Kuu ikiwa ni matukio ya  kuwaaga mitume, kushikwa, kufa na kufufuka kwa Bwana wetu Yesu Kristo.
Hiki ndicho kilikuwa kilele cha simulizi zote. Kwa namna ya pekee tunayakuta katika Injili ya Mt. Yohana sura ya 12 hadi 20, ambayo inasimulia kwa kinaganaga juma hilo kuu. Mtakatifu Yohana alikuwa shuhuha wa matukio haya yote na hadi kifo chake aliyakumbuka kwa uwazi, yalimwachia alama kubwa katika maisha yake.
Yesu Kristo alikufa na kufufuka wakati wa maadhimisho ya Pasaka ya Wayahudi. Katika siku hizo Wayahudi humkumbuka Musa na kukombolewa kwao kutoka utumwani Misri. Huadhimisha mapatano kati ya Mungu na taifa lao la  Israel.
Pasaka, yalikuwa ni maadhimisho ya juma zima, wakikumbuka na kusimilia historia yao kuanzia baba zao walipokula chakula cha mwisho huko Misri, ikiwa ni mkate bila kutiwa chachu na mboga chungu na nyama ya kondoo, ambaye damu yake  waliipaka milango yao.

SOMA ZAIDI KATIKA TUMAINI LETU.

1. Utangulizi
Kipindi cha Kwaresima kinahusika na liturujia ya kubariki mafuta na kuweka wakfu Krisma. Askofu hana budi kuwa kuhani mkuu wa kundi lake. Maisha ya Waamini wake katika Kristo, kwa namna fulani yanatokana naye na kumtegemea yeye.
Askofu huadhimisha Misa ya Krisma, pamoja na Mapadri waliotoka sehemu mbalimbali za Jimbo Lake. Katika Misa hiyo huweka wakfu Krisma na kubariki mafuta mengine. Misa hii ya Krisma ni njia mojawapo kubwa ya kuonyesha ukamilifu wa Ukuhani wa Askofu, na ni ishara ya muungano mkubwa uliopo kati ya Askofu na Mapadri wake.
Misa ya Kubariki mafuta ya Krisma, hufanyika kabla ya Misa ya Karamu ya Mwisho ya Bwana. Misa haiadhimishwi bila mkusanyiko wa Waamini. soma kwenye Tumaini Letu

DAR ES SALAAM

Na Joseph Mihangwa

Ghafla, Afrika imenyamaza kupiga kelele juu ya paa kutangaza sera zake za maendeleo zenye sura ya ubinadamu; sera zilizojaa kurasa za Vyombo vya Habari enzi za uhuru na zama za mageuzi ya uchumi kufuatia uhuru, kwa maandishi makubwa makubwa na kwa wino wa kuangaza:
“Ujamaa” kwa Tanzania; “Zambian Humanism” kwa Zambia; The Common Man’s Charter” – Uganda na “The Guinean Revolution” kwa Guinea ya Rais Ahmed Sekou Toure.

Ujenzi wa Miundo mbinu:
Mwishoni mwa mkutano waliunda Shirika lililoitwa: ‘Inter-Regional Episcopal Board of Eastern Africa (ITEBEA)’. Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu wa Zambia, Fr. Killian Flynn, OFM Cap alichaguliwa kuwa Katibu Mkuu wake wa kwanza na kuanzia mwaka 1964 akawa na ofisi ya kudumu Nairobi, Kenya.
Fr. Killian Flynn ndiye Baba wa Amecea aliyehudumu hadi mwaka 1972. Askofu Mkuu Adam Kozlowiecki, (Baadaye Kadinali) wa Lusaka, Zambia alikuwa Mwenyekiti wake wa kwanza.
Mkutano wa Pili ulikuwa huko Roma: Wakati wa Mtaguso Mkuu wa Pili wa Vatikani (1962 -65) Maaskofu walipata muda wa kufahamiana zaidi na mnamo Novemba 1964 Maaskofu walikutana Roma katika Chuo cha Mt.  Anselmo.

SOMA ZAIDI KWENYE APP AU RIFALY

VATICAN CITY, Vatican

Baba Mtakatifu Fransisko amesema kuwa mateso na mahangaiko ya mwanadamu, ni zawadi ya matumaini na uaminifu wa Mungu katika Fumbo la Pasaka, na kwamba upendo wa Mungu daima utawaandama waja wake hata wakati wa majaribu na vikwazo katika maisha yao.
Papa alitoa ujumbe huo katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Siku ya 33 ya Wagonjwa Duniani mwaka 2025, iliyoadhimishwa mjini Vatican, siku ambayo ilianzishwa Mei 13 mwaka 1992, na kuadhimishwa kwa mara ya kwanza kwenye Madhabahu ya Bikira Maria wa Lourdes nchini Ufaransa, mnamo Februari 11 mwaka 1993.
Maadhimisho ya Siku ya Wagonjwa kwa ngazi ya kijimbo yaliyoadhimishwa mwaka huu wa 2025, yananogeshwa na kauli mbiu isemayo, “Na tumaini halitahayarishi, lakini hutuimarisha wakati wa majaribu,” huku Baba Mtakatifu akiwaalika watu wote wa Mungu kuwa Mahujaji wa Matumaini.

DAR ES SALAAM

Na Dk. Felician B. Kilahama

Mitihani ya kuhitimisha Kidato cha Nne, Tanzania (CSEE) ilifanyika Novemba 11 hadi 29, 2024.
Matokeo yakatangazwa rasimi Januari 23, 2025 na Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Mitihani Tanzania (National Examinations Council of Tanzania: NECTA) Dk. Said Mohammed kupitia hafla na Waandishi wa Habari.
Taarifa iliyotolewa na Mtendaji Mkuu wa NECTA, ilionyesha kuwa ufaulu umeongezeka kwa asilimia tatu (3) kutokana na watahiniwa wengi kufaulu.
Hiyo inamaanisha kuwa kati ya watahimiwa 516,695, kati ya hao watahiniwa 477,262 wamefauli kwa madaraja: I, II, III na IV; ikiwa ni ufaulu wa asilimia 92.37 kulinganisha na matokeo ya mitihani ya 2023 yenye ufaulu wa asilimia 89.36 tu.
Kadhalika, ufaulu kwa madaraja ya I, II na III ni watahiniwa 221,952 sawa na asilimia 43, wakati mwaka 2023 walikuwa watahiniwa 197,426 sawa na asilimia 37.4 tu.
Vile vile, matokeo yameonyesha kuwa waliopata daraja la nne (iv) pamoja na waliopata alama (sufuri) wamepungua kulinganisha na matokeo ya mwaka 2023; hivyo kuashiria ongezeko la asilimia 5.6 wa ubora wa kufaulu.
Hata hivyo, Katibu Mtendaji, NECTA alibainisha kuwa kwa matokeo ya mwaka 2024, watahiniwa 67, NECTA imelazimika kufuta matokeo yao kutokana na udanganyifu wakati wakifanya mitihani.

DAR ES SALAAM

Na Alex Kachhelewa

Viongozi wa Matifa ya Afrika Mashariki (East African Community: EAC) na wale wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (Southern Africa Development Community: SADC), walikutana hivi karibuni jijini Dar es Salaam katika Mkutano Maalumu kuhusu kusaka suluhu ya mzozo wa vita nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).
Mzozo huo ni kati ya Majeshi ya Serikali ya DRC dhidi ya Vikosi vya Waasi wa Movement For March 23- au maarufu kama M23, wanaosadikiwa kuuteka Mji wa Goma, Mashariki mwa nchi hiyo.
Katika mkutano huo ambapo Rais wa DRC Felix Tshisekedi Shilombo, yeye alishiriki kwa njia ya Mtandao, Viongozi hao walifanya maamuzi yatakayosaidia kurejesha amani  katika mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), iliyogubikwa na mzozo wa muda mrefu zaidi kuwahi kushuhudiwa.
Mkutano huo uliwakaribisha viongozi hao chini ya Mwenyeji Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Samia Suluhu Hassan, uliohudhuriwa na wakuu wa nchi na serikali kutoka mataifa wanachama wa EAC na SADC,  ambao uliongozwa na Mwenyekiti wa EAC, Rais William Ruto wa Jamhuri ya Kenya, na Mwenyekiti wa SADC, Rais Emmerson Mnangagwa wa  Jamhuri ya Zimbabwe,  hapakuwapo Rais wa Congo DRC Felix Tshisekedi, ambaye alishiriki kwa njia ya mtandao.

Page 1 of 4