Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

TAFAKARI SOMO LA INJILI DOMINIKA YA 19

Amani na Salama!
“Mimi ndimi chakula cha uzima; yeye ajaye kwangu hataona njaa kabisa, naye aniaminiye, hataona kiu kamwe.” Haya ndiyo maneno ya hitimisho la somo la Injili ya Dominika iliyopita. Yesu anajitambulisha kwa wasikilizaji wake kwa namna ambayo iliwakwaza, ni maneno yaliyoweka imani yao njia panda, na hapa ndipo tunaona wasikilizaji wake ambao Mwinjili anawatambulisha kama “Wayahudi,” walimnung’unikia Yesu kutokana na maneno hayo.
Wayahudi waliamini kuwa na ukweli wote, na ndiyo Torati na Manabii. “Atamlisha mkate wa ufahamu, na kumnywesha maji ya hekima.” (Yoshua bin Sira, 15:3) Hivyo, ndiyo kusema kuwa mkate wa uzima ni Neno la Mungu ambalo Wayahudi waliamini kuwa nalo katika ukamilifu wake, ndiyo Torati na Manabii na Vitabu vingine vya Maandiko Matakatifu.
Kwao ilikuwa ni makwazo makubwa, kwani Yesu leo anajitambulisha kuwa ni Yeye aliye mkate wa uzima wa milele utokao mbinguni, ni kwa kulisikiliza na kulishika Neno lake, kila mwenye njaa na kiu atashibishwa, na hivyo hataona njaa wala kiu tena.
Wayahudi walishindwa kuupokea utambulisho wa Yesu kama chakula cha uzima, na wakabaki kumwona kama mwana wa Yusufu tu, na tena waliyemfahamu vyema hata kazi na ujira wake kuwa ni ule duni kabisa, na zaidi sana hata mama yake pia walimfahamu. Ni watu waliomfahamu vyema na vizuri, na kwa nini basi anajitambulisha na kujifananisha kuwa ni Mungu, ni kutoka mbinguni?
“Wakasema, huyu siye Yesu, mwana wa Yusufu, ambaye twamjua babaye na mamaye? Sasa asemaje huyu, ameshuka kutoka mbinguni?” Na tunasikia manung’uniko haya hawakumwelekezea Yesu, bali yalikuwepo baina yao, miongoni mwao, kati yao wenyewe.
Kunung’unika siyo kitendo kile cha kulalamika tu. Naomba kieleweke, na Mwinjili anakitumia kitenzi hicho kuonesha mkwamo wao wa kiimani, kukwazika na kujikwaa kwao kwa fundisho lenye utambulisho mpya kumhusu Yesu, utambulisho ambao unamfunua Yesu kuwa si tu mwanadamu kweli, bali pia ni Mungu kweli, ametoka kwa Mungu, amekuja kuifunua katika ukamilifu sura halisi ya Mungu. Kwao haikuwa jambo rahisi na lenye kueleweka kuwa kwa njia ya Yesu, hekima ya Mungu imejimwilisha na kukaa kati yao, na kuwa katikati yao. Soma zaidi Tumaini Letu.

Vijana Waimarishwa wa Sakramenti Takatifu ya Kipaimara wa Parokia ya Bikira Maria Mama wa Rozari Takatifu, Makongo Juu, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, wakiwa kanisani wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya kutoa Sakramenti hiyo.

Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Henry Mchamungu, akiwa katika picha ya pamoja na Mapadri na vijana waliopokea Sakramenti Takatifu ya Kipaimara katika Parokia ya Mtakatifu Rita wa Kashia – Temboni, jimboni humo, baada ya Adhimisho la Misa Takatifu. Kulia kwa Askofu, ni Paroko wa Parokia hiyo, Padri Festo Ngonyani. (Picha na Mathayo Kijazi)

Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Jude Thaddaeus Ruwa’ichi akimbariki mtoto katika Parokia ya Bikira Maria Mama wa Rozari Takatifu, Makongo Juu, wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Kipaimara iliyoadhimishwa parokiani hapo. Kulia kwa Askofu Mkuu, ni Paroko wa Parokia hiyo, Padri Joseph Massenge, na aliyesimama ni Paroko Msaidizi wa Parokia hiyo, Padri Canisius Hali.

Watoto wa Shirika la Kipapa la Utoto Mtakatifu wa Parokia ya Mwenyeheri Antonio Rosmini, Mpiji Magoe, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, wakiwa kanisani wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Kipaimara. Kushoto aliyesimama ni Mlezi wa Shirika hilo, Krista Kimalio.

Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Jude Thaddaeus Ruwa’ichi, akiwa katika picha ya pamoja na Mapadri  na Viongozi wa Halmashauri ya Walei wa Parokia ya Bikira Maria Mama wa Rozari Takatifu, Makongo Juu jimboni humo, wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Kipaimara iliyoadhimishwa hivi karibuni parokiani hapo. (Picha zote na Yohana Kasosi).

Vijana Waimarishwa wa Parokia ya Mwenyeheri Antonio Rosmini, Mpiji Magohe, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, wakiwa kanisani wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Sakramenti Takatifu ya Kipaimara iliyoadhimishwa hivi karibuni parokiani hapo.

Waamini wa Parokia ya Bikira Maria Mama wa Rozari Takatifu, Makongo Juu, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, wakiwa kanisani wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Kipaimara iliyoadhimishwa parokiani hapo hivi karibuni.

Waamini wa Parokia ya Mtakatifu Maria De Mathias, Mivumoni, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, wakiwa kanisani wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Dominika.

Wasimamizi wa Zaka wa Parokia ya Bikira Maria wa Mlima Karmeli, Bunju Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, wakiwa kanisani wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Dominika.