Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Katika safu hii ya Chimba Chimba Historia ya Kanisa wiki iliyopita, tuliwaletea historia ya Uinjilishaji katika nchi za Afrika ya Kati na Camroon. Leo tunaanza kuwaletea historia ya Uinjilishaji ulivyoingia katika nchi ya Afrika Kusini. Sasa endelea…

Nchi ya Afrika ya Kusini kabla ya Wazungu kufika huko, ilikaliwa na Wasan au Wahentoti kama Wazungu walivyowaita pamoja na Wabantu wakiwemo Wazulu, Waxhosa na wengine.

Ingawa Wareno walipita Afrika ya Kusini wakienda India, hawakuacha misioni yo yote kule. Vile vile hawakufanya koloni za kudumu huko. Wakoloni wa kudumu walifika mwaka 1650 wengi waliokosa makazi kwao wengi wao wakltoka Uholanzi, na wachache Ujerumani na Ufaransa.
 
Wote hao waliunganishwa na imani moja walikuwa Waprotestanti Wakalvinisti wenye siasa kali. Katika imani yao walijiona siyo kama watu weusi bali wao walikuwa wateule wa Bwana na matendo yao yalidhihirisha hilo.

Kwa uhakika walijua kwamba walikuwa wameokoka, walitumia Biblia (Mwa, 9) hasa simulizi juu ya Ham mtoto wa Noa, kuonyesha kwamba watu weusi walikuwa watoto wa Ham waliolaaniwa.

Hii ilikuwa dhana ya Wazungu wengi, isipokuwa dhamira na mtazamo wa uhusiano na namna ya kusaidia, ilikuwa tofauti. Comboni Mmisionari mkubwa Mkatoliki huko Sudan aliongelea juu ya kuwaombea ‘watoto maskini wa Ham,’ akitaka kuona kama nao wanaweza kukombolewa, ingawa ni vigumu.

Wakalvinisti waliongelea juu ya ‘watoto wa Ham waliolaaniwa’ na hivyo hakuna la kufanya kuwasaidia. Bahati mbaya vile vile wale Wakalvinisti wa Kanisa la Mageuzi la Uholanzi hawakuwa na sera ya Uinjilishaji kwa Waafrika kwa sababu kwao waliokoka wale tu waliopangiwa na Mungu, ambao walionyesha ishara za nje za wokovu.

Kwa Waafrika, ishara za nje, ikiwemo kuwa na wake wengi, ilionyesha kwamba hawakuchaguliwa na Mungu, na hilo mtu huwezi kuligeuza.

Nchi ya Afrika ya Kusini ilipotekwa na Waingereza miaka ya 1806-36, utumwa ulipigwa marufuku, lakini Waafrika walibaki kuwa watumishi na manamba kwa manufaa ya Wazungu. Wakalvinisti walibuni mafundisho ya dini (teolojia) ya ubaguzi mkali kwamba Mungu aliumba mtu mweusi amtumikie mzungu.

Madhehebu mengine ya Kikristu pamoja na serikali ya Uingereza walipopinga sera na mafundisho hayo ya dini, Wazungu wengine zaidi ya 6,000 wenye siasa kali walihamia kaskazini hadi Rhodesia (sasa Zimbabwe).

Huko walitaka wawe na nchi yao, ili wawe na uhuru wa kuwatumikisha Waafrika bila kubughudhiwa. Wao walijiona kama Waisraeli wa zamani, taifa teule ambalo Mungu amewatoa katika nchi ya mateso, na anawapeleka katika nchi ya agano atakayowapa.

Kuingia kwa Wamisionari Waprotestnti Afrika Kusini:
Wamisionari wa kweli wa kwanza walikuwa wa dhehebu la Moraviani kutoka Ujerumani waliofika Afrika Kusini mwaka 1792. Baadaye yalikuja mashirika mengine ambayo yalikuwa na mafanikio makubwa zaidi kama Shirika la Kimisionari la London (London Missionery Society: LMS), ambao ni Waanglikana Wainjilisti waliofika huko mwaka 1799.

Wamisionari hawa walifanya kazi kubwa sana kupigania haki za watu weusi. Kwa namna ya pekee, Dk. Yohannes van der Kemp aliyepigana sana dhidi ya ukatili wa Makaburu. Wakati huo Makanisa ya Wakaburu yalisisitiza ndani ya Kanisa kuwatenga kati ya Wazungu na Wachotara (mchanganyiko wa wazazi Wazungu na Waafrika) na kuwajengea Waafrika makanisa yao. Zaidi soma Tumaini Letu...

WASHINGTON, America
Nahodha wa timu ya Taifa ya Wales, Aaron James Ramsey, ambaye pia ni kiungo wa klabu ya Cardiff City inayoshiriki EFL Championship nchini Uingereza, amesema kuwa anaamini kwamba kuna nyakati za kusisimua mbele kwa Wales chini ya Kocha Mkuu wake mpya, Craig Bellamy.
Wales ilimteua mshambuliaji wa zamani Bellamy kwa mkataba wa miaka minne mwezi Julai, baada ya kumfuta kazi Rob Page mwezi Juni.
Kiungo wa kati wa Cardiff City Ramsey, 33, alicheza pamoja na Bellamy kwa klabu na nchi na anamuunga mkono kocha msaidizi wa zamani wa Burnley na Anderlecht, kustawi katika nafasi yake mpya.
Bellamy mzaliwa wa Cardiff, alishinda mechi 78 za Wales na kuwa nahodha wa timu kati ya 2007 na 2010, akarithiwa na Ramsey wakati huo akiwa kiungo wa Arsenal akiwa na umri wa miaka 20 pekee.
Baadaye Ashley Williams na Gareth Bale walivaa kitambaa kwa Wales kabla ya Ramsey kupewa jukumu tena baada ya kustaafu kwa Bale Januari mwaka 2023.
“Nimefurahi sana. Nimemfahamu Craig kwa miaka kadhaa sasa na nimefurahishwa naye, nina hakika atakuwa na mafanikio ya kweli. Ukiangalia timu alizoshiriki nazo na jinsi walivyocheza, kushinikiza juu, ukali, kudhibiti mchezo nadhani Wales wana mengi ya kutarajia natumai kuna nyakati za kusisimua mbeleni,” alisema Ramsey.

BARNSLEY, Uingereza
Mwingereza Molly Caudery ameondolewa katika kufuzu fainali ya mbio za kupokezana vijiti katika Michezo ya Olimpiki inayoendelea jijini Paris, Ufaransa ya mwaka huu 2024.
Caudery, bingwa wa dunia wa ndani ambaye aliweka rekodi ya Uingereza ya mita 4.92 katika hafla hiyo mwezi Juni mwaka huu, alishindwa kuvuka mita 4.55 katika uwanja wa Taifa wa Ufaransa wa mpira wa miguu, Stade de France.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 alitarajiwa kuonyeshwa vyema kwenye michezo hiyo baada ya mwaka mzuri ambapo amerekodi kanda tisa bora za kibinafsi.
Pia, alishinda shaba kwenye Mashindano ya Uropa mwezi Juni, na kumaliza wa tano kwenye Mashindano ya Dunia ya mwaka jana.
Mwanariadha wa zamani wa Uingereza wa mbio za mita 400, Katharine Merry alisema kuwa huo ni mshtuko mkubwa wa mashindano ya Olimpiki hadi sasa.
“Molly Caudery amekwenda juu ya urefu wa 4.92m [msimu huu] - 4cm juu kuliko mtu mwingine yeyote duniani,” alisema Merry.

DAR ES SALAAM

Na Ibrahim Mkamba

Tanzania ina wawakilishi wanne kwenye mashindano makubwa ya soka Afrika. Young Africans, (nitakaowataja baadaye Yanga), na Azam FC watatuwakilisha kwenye ligi ya mabingwa Afrika, huku Simba na Coastal Union wakituwakilisha kwenye mashindano ya kugombea ubingwa wa Kombe la Shirikisho Afrika.
Makala hii inaongelea hatari ya timu kujiamini kupita kiasi au kuelezewa ubora wao kupita kiasi dhidi ya wapinzani wao, tena kwa kauli zinazowafikia wapinzani hao. Hii ipo kwa Yanga na Simba, na si kwa Azam FC na Coastal Union, na ndiyo sababu makala hii itaziongelea tu timu hizo za Kariakoo, Dar es Salaam.
Ukweli haupaswi kupingika kwamba, ukisahau kucheza nusu fainali ya mashindano ya kugombea ubingwa wa Afrika mwaka 1974 kwa mfumo wa mtoano mwanzo mwisho, sahau kucheza fainali ya mashindano ya CAF mwaka 1993  na potezea kuivua ubingwa  wa Afrika Zamalek ya Misri na kutinga makundi kuwania ubingwa wa Afrika mwaka 2003, tangu mwaka 2018 mpaka sasa, Simba imekuwa moja ya timu za Afrika ya kufika hatua ya robo fainali katika mashindano makubwa ya soka ya Afrika kwa mfululizo.
Ukiiondoa Al Ahly ambayo kwao kubeba ubingwa wa Afrika si habari tena, timu nyingi kubwa za bara hili zimeshindwa kufikia hatua hiyo mfululizo miaka hii. Kuna zilizopotea kipindi fulani kama Zamalek, Esperance de Tunis, Raja Athletic Club, TP Mazembe na nyinginezo kubwa. Kwa hiyo walichofanya Simba si kidogo bali ni kikubwa kinachofanya wastahili sifa. Timu kuwa na uimara ule ule kwa misimu mitano mfululizo, ni jambo kubwa.
Yanga wamekuwa  na historia ya kusifika kwenye mashindano ya Afrika tangu 1969 walipotolewa kwenye hatua ya robo fainali kwa kura ya shilingi jijini Dar es Salaam na Asante Kotoko ya Ghana ya kipa wao Robert Mensah, na mkali wa mabao Ibrahim Sunday.
Ni Yanga ndiyo ilikuwa ya kwanza kucheza hatua ya makundi mashindano ya ligi ya mabingwa Afrika mwaka ule ule 1998 utaratibu huo ulipoanzishwa. Wakafika fainali Shirikisho Afrika msimu wa 2023/2024 na msimu uliomalizika waliishia robo fainali Afrika. Kwa sasa Yanga ni moja ya timu tishio Afrika. Hili si la kubishaniwa.
Pamoja na ukubwa walionao Yanga na Simba kwa sasa, hiyo haimaanishi watazishinda timu zote, za hadhi zozote, nyakati zote. Kama Simba walivyoifunga Al Ahly Dar es Salaam mechi mbili miaka hii ya karibuni kwa ushindi wa 1-0 kila mechi, magoli ya Meddy Kagere na Luis Miquissone ya mechi hizo tofauti, ndivyo Uhamiaji Zanzibar au wawakilishi wa Libya wanavyoweza kuitupa Simba nje ya mashindano ya Kombe la Shirikisho hatua ya awali.
Kama Yanga ilivyoipiga CR Belouizdad 4-0 jijini Dar es Salaam, ndivyo Vital’O inavyoweza kuishinda Yanga na kuitupa nje ya mashindano kwenye hatua ya awali. Yanga inaweza kupenya hapo kisha kukwama kwa SC Villa ya Uganda, au Commercial Bank ya Ethiopia.
Natoa tahadhari hizo kutokana na kauli ya kujirudiarudia ya Afisa Habari wa Yanga na ya wachambuzi kadhaa wa soka kwamba Yanga itabeba ubingwa wa soka wa Afrika msimu huu. Kwa upande mwingine, kuna baadhi ya wachambuzi wa soka husema Simba itabeba ubingwa wa Kombe la Shirikisho. Angalau kwa upande huo, Afisa Habari wa Simba hajawahi kutamba hivyo. Afadhali kwa Yanga iliyo kamili tangu msimu wa 2023/2024, lakini Simba iko kwenye matengenezo.
Madhara ya kauli za kuzipaisha Yanga na Simba kwenye ushiriki wao wa mashindano ya Afrika ni, kwanza, zinawafanya wachezaji wao wawe kwenye shinikizo kubwa wakutanapo na timu wanazoaminishwa kuwa dhaifu. Vichwani mwao hujiuliza itakuwaje wakishindwa kuwashinda wadogo hao? Kucheza kwa shinikizo, si jambo salama kwenye soka.
Pili, timu zetu zitaziendea mechi hizo katika hali ya kama kwamba zimeshashinda kwa jinsi zinavyopotoshwa. Hivyo, watabweteka, na wakishtuka tu, mambo tayari yameshakuwa magumu. Zaidi soma Tumaini Letu

Dekano wa Dekania ya Mtakatifu Gaspar na Paroko wa Parokia ya Bikira Maria wa Mlima Karmeli, Bunju, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Padri Dominick Somola, akisalimiana na Waamini wa Chama cha Moyo Mtakatifu wa Yesu wa Parokia ya Bikira Maria wa Rozari Takatifu, Makongo Juu, baada ya kushiriki Adhimisho la Misa Takatifu iliyofanyika katika Parokia ya Bunju, hivi karibuni.

Paroko mpya wa Parokia ya Bikira Maria Mama wa Mungu, Mbopo-Madale, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, (wa tatu kutoka kushoto), akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Kamati Tendaji ya Parokia hiyo, baada ya Adhimisho la Misa Takatifu ya Kumsimika Paroko huyo, iliyofanyika hivi karibuni parokiani hapo. (Picha zote na Yohana Kasosi)

Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, Askofu Mkuu Mstaafu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, akiwa na Mapadri katika picha ya pamoja na vijana 153 waliopata Sakramenti Takatifu ya Kipaimara iliyofanyika katika Parokia ya Mtakatifu Augustino, Salasala jimboni humo, baada ya Adhimisho la Misa Takatifu ya Kipaimara. Kulia kwa Kardinali ni Paroko wa Parokia hiyo, Padri Peter Assenga.

DAR ES SALAAM

Na Mathayo Kijazi

Imeelezwa kuwa hakuna kitu kinachoweza kufanywa na Waamini katika Parokia, bila kumshirikisha Askofu Mkuu, kwani vitu vyote ni mali ya Jimbo.
Kauli hiyo ilitolewa hivi karibuni na Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Stephano Musomba wakati wa homilia yake katika Adhmisho la Misa Takatifu ya Sakramenti Takatifu ya Kipaimara kwa vijana 80 wa Parokia ya Mtakatifu Teresa wa Benedicta wa Msalaba – Msumi, jimboni Dar es Salaam.
“Maeneo yote hayo mliyoyanunua, mjue kwamba ni mali ya Jimbo, sawa jamani. Kwa hiyo, msije mkaanzisha kitu chochote kile, bila kumhusisha Askofu Mkuu, kwa sababu nilisikia tetesi tetesi kwamba mnataka kununua sijui shamba la kuzikia, mkienda kienyeji bila baraka ya Askofu Mkuu, ni kosa,” alisema Askofu Musomba.
Awali, katika homilia yake Askofu huyo aliwataka wazazi kuongeza usimamizi kwa watoto wao waliopokea Sakramenti Takatifu ya Kipaimara, kwani hiyo itawasaidia watoto hao kutambua wajibu wao walioitiwa.
“Kwa hiyo wazazi na walezi, ni jukumu lenu kuongeza usimamizi kwa watoto hawa kwa sababu hiyo ndiyo njia itakayowafanya watambue wajibu wao. Hakikisheni watoto hawa wasiyumbishwe wala wasichanganywe katika imani,” alisema Askofu Musomba.
Vile vile, alisema kuwa mtoto anapopokea Sakramenti Takatifu ya Kipaimara, anatakiwa kushuhudia kile anachokiishi, kwani kwa Sakramenti hiyo, tayari ameimarika.
Aliongeza kuwa Sakramenti hiyo Takatifu ina umuhimu mkubwa kwa kila anayeipokea, kwa sababu inamkamilisha katika Neema ya Ubatizo, na kumkamilisha pia katika imani Katoliki.
Sambamba na hayo, Askofu huyo Msaidizi aliwakumbusha Wakristo kutambua kwamba zawadi ya Kristo mfufuka kwa Waamini wake, ni amani.
Wakati huo huo, Askofu huyo, aliwasihi Waamini wa Parokia ya Msumi kumshukuru Mungu, kwani kupitia Adhimisho hilo la Misa Takatifu, wamepata Wakristo wengine 80 waliokomaa ambao ni Waimarishwa.
Aliwashukuru Waamini wa Parokia hiyo kwa kuwachangia Skauti Shilingi laki 3 kwa ajili ya Kongamano lao linalotarajia kufanyika jimboni humo.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Parokia hiyo, Frank Werema, katika risala yake, alisema kuwa miongoni mwa mambo wanayoendelea kuyafanya kiroho, ni pamoja na kuwahamasisha Waamini ambao bado hawajafunga ndoa, wafunge, kwani kaya zaidi ya 482, wakazi wake hawajafunga ndoa.
Akizungumzia changamoto zinazowakabili hadi sasa parokiani hapo, Mwenyekiti huyo alisema kwamba kubwa ni ubovu wa miundombinu ya barabara katika maeneo ya Parokia hiyo.
Naye Mwandishi Laura Chrispin, anaripoti kuwa, Watoto wanaopokea Sakramenti Takatifu ya Kipaimara wametakiwa kufahamu kuwa wanampokea Roho Mtakatifu kwa mara ya pili atakayewaongoza siku zote za maisha yao.
Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Stephano Musomba wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Sakramenti Takatifu ya Kipaimara iliyofanyika katika Parokia ya Mtakatifu Martha -Mikocheni, alisema kuwa hata kipindi cha Mitume kabla ya kumpokea Roho Mtakatifu, Mitume mara zote walikuwa ni watu wa kuuliza maswali lakini baada ya kumpokea Roho Mtakatifu, walikuwa ni watu wa ushuhuda zaidi.
Hiyo ikiwa ni kama funzo kwenu kuwa inawapasa kuwa ni watu wa kumshuhudia Kristu kwa matendo yenu wenyewe, pamoja na kueleza makuu ya kristu kwa watu wengine.
Alisema hata katika Sinodi ya Maaskofu, inatuelekeza kutembea pamoja na kuwataka wengine wasibaki nyuma bali kutembea pamoja, ndiyo maana ukisema Kanisa la Kisinodi unaseama Ushirika na Ushiriki wa Kimisionari.
Katika Ushirika hawa ni Wanajumuiya, Wanafamilia ambayo kuna huduma wana hudumiana na kufanya kazi zote kwa pamoja na ni washiriki, ndo mana wanakuwa Wamisionari.
Mhashamu Musomba alisema “Roho Mtakatifu anavyokuja kwetu, anatufanya tuzungumze Lugha moja, hiyo ambayo ni katika upendo zaidi”.
Askofu Musomba aliwataka Waamini kuwa na amani katika familia zao na kumwomba zaidi Mungu awaepushe na dhambi kwani dhambi ni mojawapo ya sababu inayopelekea kupotea kwa amani.
Aidha, aliwataka Waamini kutosahau baadhi ya dhambi, hasa dhambi ya jamii ambayo ni kwa mtu yeyote anaweza kufanya mfano kwa wafanya biashara kutengeneza chakula kwa uchafu na kusababisha magonjwa kwa jamii, hiyo ni dhambi na inakupasa kuiungama mara moja.
Askofu Musomba alitoa wito kwa wazazi na walezi kwa kuwataka wasaidie kuwasindikiza katika imani moja ya Kanisa Katoliki, na siyo kuwachanganya watoto katika imani zingine.

DAR ES SALAAM

Na Mwandishi wetu

Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, Askofu Mkuu Mstaafu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, amewataka Waamini wamtangulize Mungu, wanapofanya jambo lolote, ili wapate neema kamili.
Kardinali Pengo alisema hayo katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Sakramenti ya Kipaimara kwa vijana 150, iliyofanyika katika Parokia ya Mtakatifu Augustino – Salasala, jimboni Dar es Salaam.
“Watu wengi huwa wanapenda kujifanyia mambo wanayoyajua wao, na kuamua kumuacha Mungu. Ukijifanyia kitu bila kumtanguliza Mungu huwezi kufanikiwa,” alisema Kadrinali Pengo na kuongeza, “Hata kama unatamani na wewe uje kuwa Rais wa Taifa hili la Tanzania, au unataka uje kuwa mfanyabiashara mkubwa katika nchi hii, lazima umtangulize Muumba wako ambaye ni Mungu Baba iliyekubariki ili uweze kufaulu vizuli.”
Aliwasihi vijana waliopokea Sakramenti Takatifu ya Kipaimara kufahamu kwamba, sasa wamekuwa Wakristo kamili, akiwasisitiza kuyazingatia mafundisho ya Kanisa ili waendelee kudumu katika imani.
Kwa upande wake Paroko wa Parokia hiyo, Padri Peter Assenga aliwaomba wazazi na walezi wa vijana hao wasihame imani yao Katoliki, kwani ndiyo imani ya kweli.
Alimshukuru Kardinali Pengo kwa kuwapatia vijana hao Sakramenti Takatifu ya Kipaimara.
Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Walei wa parokia hiyo, Boniface Ngowi alisema kuwa kwa sasa Parokia hiyo imepata mafanikio makubwa, kwani wamejenga kanisa jipya kubwa ambalo lilitabarukiwa na Kardinali Pengo, alisema kuwa wao kama Parokia, wamejenga nyumba kubwa ya kisasa ambayo ilibarikiwa na kuzinduliwa na Askufu Mkuu wa Jimbo hilo, Mhashamu Jude Thaddaeus Ruwa’ichi.

KIGOMA

Na Mwandishi wetu

Waziri wa Kilimo Hussein Bashe amewahakikishia Watanzania kuwa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan amedhamiria kuleta mapinduzi kwenye Sekta ya Umwagiliaji, hivyo miradi yote aliyoahidi itatekelezwa.
Waziri Bashe alisema hayo wakati akizungumza na wadau wa umwagiliaji katika eneo la mradi wa Luiche, ambapo amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kufanikisha utekelezaji  wa mradi huo.
“Leo tumefanya uzinduzi wa Mradi Mkubwa wa Umwagiliaji katika Bonde la Luiche Wilayani Kigoma katika Mkoa wa Kigoma. Miradi hiyo yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 60 itakwenda kunufaisha zaidi ya wakulima 9312 kupitia Kilimo cha Umwagiliaji,”alisema Bashe.
Waziri Bashe alisisitiza kwamba utekelezaji wa miradi hiyo unaofanywa na Tume ya Taifa ya Umwagiliaji, si hadithi, bali umelenga  kuinua Sekta ya Kilimo cha Umwagiliaji, na kuchochea ukuaji wa uchumi nchini.
Aliitaka Tume ya Taifa ya Umwagiliaji kujipanga kuhakikisha wanatekeleza miradi hiyo, na wananchi wapuuze wanaowalaghai kuuza mashamba.
Aliongeza kuwa wizara inamshukuru Rais Dk. Samia kwani anafanya kwa vitendo na hataki utani katika kilimo cha umwagiliaji.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji, Raymond Mndolwa alimshukuru Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa kufanikisha utekelezaji wa mradi wa Bonde la Luiche, ambao umekuwa ukizungumzwa tangu nchi ilipopata Uhuru, na kwamba uwekezaji huo mkubwa uliofanywa na serikali unakwenda kuleta mapinduzi makubwa kiuchumi kwa wananchi wa Kigoma.
Mndolwa pia ametumia fursa hiyo kupokea maagizo ya Waziri wa Kilimo.
“Mradi huu ni mkubwa na utazingatia uwekaji wa miundo mbinu muhimu kama barabara na itazingatia kulinda vyanzo vya maji na mazingira”, alisema Mndolwa.
Mndolwa pia aliongeza kuwa Tume ilipokea maelekezo ya Serikali  kuwa mradi ujumuishe ujenzi wa   ghala, nyumba ya watumishi, pamoja na Ofisi ya Umwagiliaji.
Akiwasilisha Taarifa ya Umwagiliaji kwa Mkoa wa Kigoma, Mhandisi Umwagiliaji Mkoa wa Kigoma, Katuta Mustang, alisema kwamba Mkoa wa Kigoma una eneo linalofaa kwa umwagiliaji lenye ukubwa wa hekta 147,000 ukiwa na skimu 59 za umwagiliaji skimu 6 pekee ndizo zilizoendelezwa.
Naye Mkuu wa Wilaya ya Kigoma, Salum Kalli alisema serikali itahakikisha ulinzi wa mradi huo.
Akimkaribisha Waziri wa Kilimo, Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto Thobias Andengenye, aliishukuru serikali kwa uwekezaji Mkubwa unaofanywa katika Mkoa wa Kigoma, kupitia kilimo cha umwagiliaji.
Mbunge wa Jimbo la Kigoma Mjini, Ngenda Shabani Kirumbe,alimshukuru raid Dk. Samia Suluhu Haasan kwa kufanikisha utekelezaji wa Mradi wa Luiche.
Mradi wa Luiche upo katika wilaya ya kigoma, mkoa wa Kigoma. Mradi huu unajumuisha vijiji vya Kamara, Simbo, Kaseke, Nyamori, Msimba, Matiazo pamoja na Kagera. Mradi huu utakuwa na  ya hekta 3000 zitakazomwagiliwa baada ya ujenzi kukamilika. Mradi huu wa Luiche umegawanyika katika mikataba miwili ambayo ni Mkataba wa ujenzi wa bwawa pamoja na mkataba wa ujenzi wa skimu ya umwagiliaji.