Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha
Makala

Makala (69)

Na  Askofu Mstaafu Method Kilaini

Wahuni:    
Wahuni walikuwa wapiganaji wakali sana, na ndio walioleta matatizo yaliyozusha uvamizi. Wahuni walikuwa watu wa Mashariki ya mbali (Mongoliani, waasia wa ngozi ya njano). Wahuni walikuwa wachungaji wakiishi Kaskazini ya Milima ya Himalaya. 

Malisho yalipoisha, hawa wapanda farasi, walianza kuvamia nchi nyingine. Mwaka 200 Baada ya Kristo (BK), walikwea ukuta wakaivamia China na kusambaratisha himaya yake, na tangu hapo ikawa nyakati za giza kwa miaka 400 iliyofuata kwa China. 

MWANZA

Na Paul Mabuga

Mjadala wa “Uswahili ni nini”, uliibuliwa hivi karibuni na mchambuzi Maggid Mjengwa, akirejea fikra za Jenerali Twaha Ulimwengu na marehemu Edwin Mtei. 
Swali hili limezua taharuki chanya: Je, Mswahili ni nani katika ulimwengu wa leo? Je, bado ni yule “muongo muongo” aliyemchukiza Mtei, au ni utambulisho uliopata sura mpya, kuanzia mitaa ya Dar es Salaam hadi jijini Berlin?
Jenerali Ulimwengu, akizungumza hivi karibuni, katika makiwa ya marehemu Edwin Mtei, alifungua ukurasa wa kumbukumbu uliosisimua wengi. 
Alieleza kuwa Mzee Mtei alikuwa na msimamo usioyumba, dhidi ya kile alichokiita “Uswahili.” Katika muktadha wa kujiuzulu kwake Uwaziri, Mtei aliamini kuwa mfumo wa “Uswahili”, ulikuwa kikwazo kwa uadilifu wa kitaifa.

Na Mwandishi Wetu

Katika makala haya kuhusu Ubatizo wa Bwana, Mwadhama Protace Kardinali Rugambwa katika mahubiri yake, ametumia fursa hii kufafanua alama muhimu, zilizojionesha wakati Kristo Yesu alipobatizwa mtoni Yordani.

Anasema kwamba alama ya kwanza ni Maji: Alama ya kifo na uhai; Mbingu zikamfunukia, Roho Mtakatifu akashuka juu yake kama hua; Alama ya pili ni kufunguka kwa mbingu; Alama ya mabadiliko ya ndani ya mwanadamu, mbele ya Mwenyezi Mungu; Alama ya tatu ni Roho Mtakatifu aliyemshukia Kristo Yesu na sauti ya Baba wa milele ikasikika: Huyu ni mwanangu, mpendwa wangu.

Ubatizo ni sakramenti inayotuingiza katika Ukristo, ni sakramenti inayotuondolea dhambi ya asili na adhabu zake zote. Ni kwa njia ya Ubatizo tunazaliwa upya kwa maji na Roho Mtakatifu, na hivyo tunakuwa ni watoto wa Mungu na wa Kanisa.

Na Dkt. Felician B. Kilahama

Namshukuru Mwenyezi Mungu aliye mwingi wa rehema, aliyeumba wanadamu kwa sura na mfano wake. Hili ni “wazo mbadala”, ikimaanisha kwamba kuna kinachotakiwa kufanyika, lakini katika harakati za utekelezaji likajitokeza ‘wazo mbadala’.
Uchaguzi Mkuu ulifanyika Oktoba 29, 2025, na aliyekuwa mgombea urais kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Mheshimiwa Dk. Samia Suluhu Hassan, akatangazwa mshindi na kuapishwa rasmi Jumatatu, Novemba 3, 2025.
Baada ya zoezi hilo kukamilika, Rais aliunda Baraza la Mawaziri, ambalo pamoja na Wakuu wa Mikoa, Wilaya, Viongozi wakuu wa Halmashauri husika, kwa pamoja inakuwa Serikali inayoongozwa na Rais.
Wakati wa kampeni za uchaguzi, kuna sehemu ambazo wananchi waliomba serikali itakayoundwa, kuanzisha wilaya na halmashauri mpya, ili kuwarahisishia wananchi kupata huduma wanazohitaji, ikiwemo kutatuliwa kero haraka iwapo ofisi husika zitakuwa karibu.

Dar es Salaam

Na Dk. Felician B. Kilahama

Mapokeo ya kihistoria tangu miaka ya 1880, yanathibitisha kwamba baadhi ya mataifa barani Ulaya mathalani, Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, Ubelgiji na Hispania, yaliweza kufika barani Afrika.
Hivyo, 1884 kukafanyika kikao maalumu jijini Berlin-Ujerumani, kwa lengo mahususi kugawana maeneo kuitawala Afrika.
Kwa upande wa Afrika-Mashariki, Wajerumani wakatawala “Tanganyika” na wakaweza kufika maeneo ya Iringa, ambako Hifadhi-Ruaha inapatikana. Wakiwa huko waliona sehemu imesheheni rasilimali nyingi za wanyamapori, na kuifananisha na “Bustani ya Edeni”.
Kiuhalisia Ruaha kuna urithi wa aina yake, mathalani milima na mabonde pamoja na rasilimali-misitu aina ya miombo, misitu inayostawi kandokando ya mito, na Mto Ruaha-Mkuu. Mto huu ni msaada mkubwa aina yake, ikiwemo wanyamapori wanaoishi kwenye hifadhi ya Ruaha.

MWANZA

Na Paul Mabuga

Hebu vuta picha: Zamani kijana wa Kitanzania hakukurupuka tu kuitwa mzazi. Kulikuwa na mifumo madhubuti ya Jando, Unyago, na yale mafunzo ya kando ya moto kutoka kwa babu na bibi, yaliyomjenga mtu kifikra na kihisia. 
Lakini leo, “moto” pekee unaowaunguza vijana wetu ni wa data za simu, na mianga ya mitandao ya kijamii. Wakati mifumo hiyo ya kijadi ikipumzika kwenye makaburi ya historia, tunapaswa kujiuliza kwa uchungu: Je, vijana wetu wanajifunza wapi kuwa wazazi?

Dar es Salaam

Na Joseph Mihangwa

Chimbuko la Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ni Mapinduzi ya Zanzibar, yaliyofanyika Visiwani humo Januari 12, 1964. 
Bila Mapinduzi hayo tusingezaliwa Tanzania, wala Chama tawala cha sasa - Chama cha Mapinduzi (CCM), ambacho ni Muungano wa Vyama vya Tanganyika African National Union (TANU) cha Tanganyika, na Afro-Shirazi Party (ASP) cha Zanzibar.
Chama kilichozaliwa Februari 5, 1977, miaka 13 baada ya Muungano uliofikiwa Aprili 26, 1977, ni matokeo ya kero za Muungano.
Mapinduzi haya yaliyoshangaza dunia kwa staili yake, yalifanyika kwa harakati za siasa za mrengo wa Kikomunisti, na kutia hofu nchi za Magharibi, hasa Marekani na Uingereza, zikaamua kuingilia kati kuyadhibiti Mapinduzi hayo, kuzuia kuenea kwa Ukomunisti Afrika kupitia Afrika Mashariki.

Katika safu hii ya Chimba Chimba Historia ya Kanisa wiki iliyopita, tuliendelea kuwaletea historia ya mitaguso mikuu, kwa kuendelea na Mtaguso Mkuu wa Kostantinopole. Leo tunawaletea historia ya kuasi kwa Kanisa la Wakopti Misri, na historia ya Mababa wa Kanisa wa Magharibi. Sasa endelea…

Bahati mbaya, Wakristo wa Misri ambao kabla walikuwa kila mara wanashinda, na hivyo wakajiona kama watetezi imara wa imani, mara hii waliposhindwa hawakufurahi. Walishinda wakati wa Arius na walishinda wakati wa Nestorius, lakini sasa kwa kusisitiza mno umoja na umungu wa Kristo walishindwa. 

Hawakupokea kushindwa, hivyo Kanisa zima likaendelea na uzushi huo ulioitwa ‘Monophysitism’, maana yake Yesu  ni Mungu na utu wake umekandamizwa. 

Mwanza

Na Paul Mabuga

Maandishi yaliyoandikwa kwenye bajaji zetu, ambayo  kwa  muhtasari na kwa  muktadha wa yaliyokusanywa katika makala haya, unaweza kusema ni kama kutoka, “Enzi za Mwalimu” hadi “Kwenye Ndoa Yenu...”:, na vilevile ni maneno yanayosema mengi yenye kusisimua, kuibua hisia, kufurahisha na hata kufikirisha, sembuse kutia hofu na kuogofya.

Ni kwamba licha ya barabara za miji yetu hapa nchini, kujaa watu na shamrashamra za kelele za honi, lakini  pia zimesheheni  falsafa ya Mswahili.. Sio kwenye vitabu au kwenye mikutano ya hadhara, bali kwenye mabango madogo yaliyobandikwa, au kuandikwa nyuma ya magari yetu ya usafiri, na vyombo vingine maarufu kama Bajaji.

Dar es Salaam

Na Pd. Richard Mjigwa- C.PP.S

Ilikuwa ni Novemba 8, mwaka 1984, Mtakatifu Yohane Paulo II (Papa), alipochapisha Waraka unaojulikana kama “Tot tantaeque” yaani “Bikira Maria ameidhinishwa kuwa Mlinzi na Mwombezi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania”, Sherehe inayoadhimishwa kitaifa kila mwaka ifikapo Desemba 9.
Katika mkesha wa uhuru wa Tanganyika, Mtakatifu Yohane XXIII, alitunga Sala Maalumu kwa ajili ya kuiombea Tanganyika, ili uhuru wake uweze kuwanufaisha watu wake.

Page 1 of 5