Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

MWANZA

Na Paul Mabuga

Hebu vuta picha: Zamani kijana wa Kitanzania hakukurupuka tu kuitwa mzazi. Kulikuwa na mifumo madhubuti ya Jando, Unyago, na yale mafunzo ya kando ya moto kutoka kwa babu na bibi, yaliyomjenga mtu kifikra na kihisia. 
Lakini leo, “moto” pekee unaowaunguza vijana wetu ni wa data za simu, na mianga ya mitandao ya kijamii. Wakati mifumo hiyo ya kijadi ikipumzika kwenye makaburi ya historia, tunapaswa kujiuliza kwa uchungu: Je, vijana wetu wanajifunza wapi kuwa wazazi?

Dar es Salaam

Na Joseph Mihangwa

Chimbuko la Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ni Mapinduzi ya Zanzibar, yaliyofanyika Visiwani humo Januari 12, 1964. 
Bila Mapinduzi hayo tusingezaliwa Tanzania, wala Chama tawala cha sasa - Chama cha Mapinduzi (CCM), ambacho ni Muungano wa Vyama vya Tanganyika African National Union (TANU) cha Tanganyika, na Afro-Shirazi Party (ASP) cha Zanzibar.
Chama kilichozaliwa Februari 5, 1977, miaka 13 baada ya Muungano uliofikiwa Aprili 26, 1977, ni matokeo ya kero za Muungano.
Mapinduzi haya yaliyoshangaza dunia kwa staili yake, yalifanyika kwa harakati za siasa za mrengo wa Kikomunisti, na kutia hofu nchi za Magharibi, hasa Marekani na Uingereza, zikaamua kuingilia kati kuyadhibiti Mapinduzi hayo, kuzuia kuenea kwa Ukomunisti Afrika kupitia Afrika Mashariki.

Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Henry Mchamungu akibariki vipaji wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Mkesha wa Mwaka Mpya 2026, katika Parokia ya Bikira Maria Mama wa Huruma - Mbezi Beach, jimboni humo. (Picha na Mathayo Kijazi) 

Vijana Wakatoliki Wafanyakazi (VIWAWA) Jimbo Kuu la Dar es Salaam wakishangilia jambo wakati wa Homilia katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Beach Mass iliyoadhimishwa ufukweni Jimbo Katoliki la Bagamoyo.

Mwenyekiti wa Parokia ya Mtakatifu Kamili Yombo Kiwalani Josephat Moshi, akiwa katika picha ya pamoja na Wanakwaya wa Kwaya ya Shirikisho ya parokia hiyo, baada ya Adhimisho la Misa Takatifu ya Krismasi iliyofanyika parokiani hapo.

Masista wa Shirika la Mtakatifu Fransisko wa Asizi Dada Wadogo Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, wakiwa katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Nadhiri za Kwanza iliyofanyika katika Nyumba ya Masista hao Mbagala jimboni humo.

DAR ES SALAAM

Na Nicholas Kilowoko

Siku chache mara baada ya pambano lililomalizika, kwa Hassan Mwakinyo kumtandika bondia Stanley Eribo kutoka nchini Nigeria kwa ‘KO’, katika raundi ya pili ya pambano la raundi 10, bondia Twaha Kiduku ameubeza ushindi wake.
Bondia Twaha alisema kuwa pambano hilo lililofanyika siku ya Boxing Day, lilikuwa halina hadhi kutokana na mpinzani wa bondia mwenzake Mwakinyo, kutokuwa katika kiwango kinachotakiwa.

DAR ES SALAAM

Na Nicholas Kilowoko

Kocha wa vijana wa klabu ya soka ya Simba, John Bocco, ameelezea mikakati yake mipya ya kuisaidia timu yao kubwa, kupata vijana wazawa wenye vipaji na watakaolisaidia Taifa pia.
Kwa muda mrefu nyota huyo wa zamani, ambaye alifanya makubwa ndani ya klabu ya Simba, Azam FC, na JKT Tanzania, alikuwa yupo kimya mara baada ya kumaliza kazi yake ya uchezaji.

DAR ES SALAAM

Na Arone Mpanduka

Mkuu wa Kitengo cha Habari cha klabu ya soka ya Azam FC, Thabit Zacharia maarufu kama Zaka Zakazi, amesema kuwa kitakwimu winga wa Taifa Stars Simon Msuva, bado ataendelea kuwa juu katika ufungaji wa mabao mengi katika kikosi hicho, kuliko mchezaji mwingine yoyote.
Akitoa ufafanuzi kuhusiana na ubishani unaoendelea, wa kumlinganisha Msuva na mchezaji wa zamani wa Taifa Stars Mrisho Ngassa, Zaka alisema kwamba nyota hao wanalinganishwa kimakosa, kwa sababu Msuva ana mabao 21 aliyoifungia Taifa Stars pekee, huku Ngassa mabao yake yakichanganywa na aliyoifungia Kilimanjaro Stars, ambayo ni ya Tanzania Bara pekee.

London, Uingereza
Meneja wa Arsenal Mikel Arteta, amekiri kuwa watakuwa wakiangalia kwa makini usajili unaowezekana, wakati wa dirisha la uhamisho la Januari.
The Gunners walitumia takribani pauni milioni 250 msimu huu wa joto, na kuleta wachezaji wapya nane, huku wakitafuta kuongeza ubora katika kikosi chao, ili kukabiliana na orodha ya mechi zilizojaa, na kushindania mataji katika mashindano mengi.
Msimu uliopita kampeni ya Arsenal iliharibiwa na majeraha, kwani walikuwa bila mlinzi Gabriel Magalhaes, kwa sehemu ya mwisho ya msimu na walicheza na kiungo Mikel Merino, kama mshambuliaji wa muda, walipomaliza wa pili katika Ligi Kuu kwa msimu wa tatu mfululizo, na walitolewa katika nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa na Paris St-Germain.
Msimu huu The Gunners pia wamekuwa wakisumbuliwa na majeraha, mara baada ya kumpoteza Kai Havertz tangu siku ya ufunguzi, huku nahodha Martin Odegaard na Bukayo Saka, Gabriel Martinelli, Noni Madueke na Max Dowman wakiwa wamekosa nafasi.
Sasa baada ya majeraha kuwaathiri zaidi wachezaji washambuliaji, ni safu ya nyuma ya Arsenal inayoteseka, Arteta alilazimika kumchezesha Declan Rice, katika nafasi isiyojulikana ya beki wa kulia dhidi ya Brighton siku ya Jumamosi, kwa sababu Jurrien Timber alikuwa majeruhi, na Riccardo Calafiori alipata tatizo wakati wa mazoezi ya kupasha misuli.