Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Waamini kutoka Parokia mbalimbali za Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, wakiwa katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Nadhiri za Kwanza za Masista wa Shirika la Mtakatifu Fransisko wa Asizi Dada Wadogo, iliyofanyika katika Makao Makuu ya Shirika hilo, Mbagala-Dar es Salaam.

Watoto wa Shirika la Kipapa la Utoto Mtakatifu kutoka Parokia mbalimbali za Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, wakiwa katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Sherehe ya Watoto Mashahidi iliyofanyika katika viwanja vya Parokia ya Kristo Mfalme, Tabata jimboni humo hivi karibuni.

Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Sana Jude Thaddaeus Ruwa’ichi (aliyeshika Fimbo ya Kichungaji), Askofu Msaidizi wa Jimbo hilo, Mhashamu Henry Mchamungu (kushoto), Askofu wa Jimbo Katoliki la Bagamoyo Mhashamu Stephano Musomba (kulia) na Mapadri wakiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Shirika la Masista wa Mtakatifu Fransisko wa Asizi Dada Wadogo na Masista walioweka Nadhiri za Kwanza, baada ya Adhimisho la Misa Takatifu ya Nadhiri hizo.

MWANZA

Na Paul Mabuga

Hebu vuta picha: Zamani kijana wa Kitanzania hakukurupuka tu kuitwa mzazi. Kulikuwa na mifumo madhubuti ya Jando, Unyago, na yale mafunzo ya kando ya moto kutoka kwa babu na bibi, yaliyomjenga mtu kifikra na kihisia. 
Lakini leo, “moto” pekee unaowaunguza vijana wetu ni wa data za simu, na mianga ya mitandao ya kijamii. Wakati mifumo hiyo ya kijadi ikipumzika kwenye makaburi ya historia, tunapaswa kujiuliza kwa uchungu: Je, vijana wetu wanajifunza wapi kuwa wazazi?

Dar es Salaam

Na Joseph Mihangwa

Chimbuko la Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ni Mapinduzi ya Zanzibar, yaliyofanyika Visiwani humo Januari 12, 1964. 
Bila Mapinduzi hayo tusingezaliwa Tanzania, wala Chama tawala cha sasa - Chama cha Mapinduzi (CCM), ambacho ni Muungano wa Vyama vya Tanganyika African National Union (TANU) cha Tanganyika, na Afro-Shirazi Party (ASP) cha Zanzibar.
Chama kilichozaliwa Februari 5, 1977, miaka 13 baada ya Muungano uliofikiwa Aprili 26, 1977, ni matokeo ya kero za Muungano.
Mapinduzi haya yaliyoshangaza dunia kwa staili yake, yalifanyika kwa harakati za siasa za mrengo wa Kikomunisti, na kutia hofu nchi za Magharibi, hasa Marekani na Uingereza, zikaamua kuingilia kati kuyadhibiti Mapinduzi hayo, kuzuia kuenea kwa Ukomunisti Afrika kupitia Afrika Mashariki.

Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Henry Mchamungu akibariki vipaji wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Mkesha wa Mwaka Mpya 2026, katika Parokia ya Bikira Maria Mama wa Huruma - Mbezi Beach, jimboni humo. (Picha na Mathayo Kijazi) 

Vijana Wakatoliki Wafanyakazi (VIWAWA) Jimbo Kuu la Dar es Salaam wakishangilia jambo wakati wa Homilia katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Beach Mass iliyoadhimishwa ufukweni Jimbo Katoliki la Bagamoyo.

Mwenyekiti wa Parokia ya Mtakatifu Kamili Yombo Kiwalani Josephat Moshi, akiwa katika picha ya pamoja na Wanakwaya wa Kwaya ya Shirikisho ya parokia hiyo, baada ya Adhimisho la Misa Takatifu ya Krismasi iliyofanyika parokiani hapo.

Masista wa Shirika la Mtakatifu Fransisko wa Asizi Dada Wadogo Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, wakiwa katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Nadhiri za Kwanza iliyofanyika katika Nyumba ya Masista hao Mbagala jimboni humo.

DAR ES SALAAM

Na Nicholas Kilowoko

Siku chache mara baada ya pambano lililomalizika, kwa Hassan Mwakinyo kumtandika bondia Stanley Eribo kutoka nchini Nigeria kwa ‘KO’, katika raundi ya pili ya pambano la raundi 10, bondia Twaha Kiduku ameubeza ushindi wake.
Bondia Twaha alisema kuwa pambano hilo lililofanyika siku ya Boxing Day, lilikuwa halina hadhi kutokana na mpinzani wa bondia mwenzake Mwakinyo, kutokuwa katika kiwango kinachotakiwa.