Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

DAR ES SALAAM

Na Arone Mpanduka

Mchezo wa skwashi ulianzishwa karne ya 19 nchini Uingereza. Ulianza kama mabadiliko ya mchezo wa racquetball, na kuendelezwa katika shule za wasichana na wavulana. 
Mchezo huu ulienea haraka katika nchi za Uingereza, kisha ulienea duniani kote, hasa katika nchi zilizoathiriwa na Wazungu kama Canada, Marekani, Australia, na baadhi ya nchi za Afrika.

DAR ES SALAAM

Na Remigius Mmavele

Rigobert Bamundele Ifoli, maarufu kwa jina  Rigo Star, alizaliwa Agosti 28,1955 jijini Kinshasa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).Rigo Star ni mpiga gita hodari aliyetikiza duniani kwa kupiga chombo hicho, alianza kuonyesha uwezo wake akiwa na umri mdogo ambapo alikuwa mmoja wa wapiga gitaa wenye ushawishi mkubwa nchini mwake.

Katika safu hii ya Chimba Chimba Historia ya Kanisa wiki iliyopita, tuliendelea kuwaletea historia ya mitaguso mikuu, kwa kuendelea na Mtaguso Mkuu wa Kostantinopole. Leo tunawaletea historia ya kuasi kwa Kanisa la Wakopti Misri, na historia ya Mababa wa Kanisa wa Magharibi. Sasa endelea…

Bahati mbaya, Wakristo wa Misri ambao kabla walikuwa kila mara wanashinda, na hivyo wakajiona kama watetezi imara wa imani, mara hii waliposhindwa hawakufurahi. Walishinda wakati wa Arius na walishinda wakati wa Nestorius, lakini sasa kwa kusisitiza mno umoja na umungu wa Kristo walishindwa. 

Hawakupokea kushindwa, hivyo Kanisa zima likaendelea na uzushi huo ulioitwa ‘Monophysitism’, maana yake Yesu  ni Mungu na utu wake umekandamizwa. 

Bagamoyo

Na Laura Mwakalunde

Askofu wa Jimbo la Bagamoyo, Mhashamu Stephano Musomba, amewataka Waamini kutokuwa na Roho dhaifu, za kushindwa kuvumilia shida na matatizo.
Askofu Musomba alisema hayo hivi karibuni, wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Dominika ya Tatu ya Furaha ya Majilio, iliyofanyika katika Parokia ya Bikira Maria wa Mlima Karmeli-Bunju, jimboni humo.

Mgeta

Na Angela Kibwana

Zaidi ya watoto Wamisionari 300 wa Shirika la Kipapa, Dekania ya Mgeta Jimboni Morogoro, wameshiriki Kongamano la kufunga mwaka, katika dekania hiyo.
Kongamano hilo limefanyika katika Parokia ya Bikira Maria wa Mlima Karmeli-Mgeta, Morogoro, likihusisha watoto kutoka Parokia sita zinazounda Dekania hiyo, kama njia mojawapo ya kuwakuza watoto kiimani na kimaadili, kupitia mafundisho ya semina na michezo mbalimbali.

Dar es Salaam

Na Laura Mwakalunde

Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Sana Jude Thaddaeus Ruwa’ichi, amewataka Waamini kutambua kwamba, Karamu ya Sakramenti Takatifu haikuja ili kushibisha tumbo.
Askofu Ruwa’ichi alisema hayo hivi karibuni, wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya kuzindua Mnara wa Kanisa, iliyofanyika Parokia ya Mwenyeheri Anuarite-Makuburi, jimboni humo.

Morogoro

Na Angela Kibwana

Mhashamu Askofu Lazarus Vitalis Msimbe -SDS, wa Jimbo Katoliki Morogoro, ameongoza Misa Takatifu ya Sherehe ya Bikira Maria Mkingiwa dhambi ya asili, Msimamizi wa Jimbo hilo, na kuwataka Waamini jimboni humo kukimbilia maombezi yake mara kwa mara, ili Jimbo liweze kustawi kiroho na kimaendeleo.
Adhimisho hilo lilifanyika katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Patris, jimboni Morogoro, iliyokwenda sambamba na kufunga mwaka Mtakatifu wa Jubilei ya matumaini miaka 2025, jozi 44 za ndoa Takatifu, pamoja na kutoa shukrani kwa Mungu, kwa mavuno ya Tegemeza Jimbo mwaka huu 2025.

Kisarawe – Pwani

Na Mathayo Kijazi

Chansela wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Padri Vincent Mpwaji, amewaalika Wakristo kutafakari na kutambua kwamba jukumu lao la kwanza la msingi, ni kuwa Mashahidi wa Yesu Kristo.
Padri Mpwaji aliyasema hayo katika homilia yake, wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Sakramenti ya Kipaimara kwa vijana 21, katika Parokia ya Mtakatifu Joseph Cottolengo – Masaki - Kisarawe, jimboni humo.

Dar es Salaam

Na Mathayo Kijazi

Imeelezwa kuwa kila anayepokea Sakramenti Takatifu ya Kipaimara, anatumwa kuwa Mkristo kweli aliye tayari kuacha dhambi na kumrudia Mungu, huku akiwa mtu wa toba.
Hayo yalisemwa na Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Henry Mchamungu, wakati wa homilia yake katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Sakramenti ya Kipaimara kwa vijana 72, katika Parokia ya Mtakatifu Maria Magdalena – Kimara Mtoni, jimboni humo.

LILONGWE, Malawi
Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Lilongwe, nchini Malawi, Mhashamu Vincent Frederick Mwakhwawa, amewataka Waamini kudumisha heshima na uvumilivu wakati wa Misa, akisisitiza kwamba sherehe ya Ekaristi haipaswi kukatizwa kamwe, hata wakati wa changamoto.
Wito huo aliutoa hivi karibuni wakati wa ziara yake ya Kitume, katika Parokia ya Mtakatifu Paulo - Namitete, jimboni humo, ambapo yeye binafsi aliwashukuru na kuwatia moyo washiriki wa Utoto Mtakatifu (Watoto wa Wamisionari).