Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

DAR ES SALAAM

Na Arone Mpanduka

Licha ya timu nne za Ligi Kuu kuwa nyuma ya ratiba, kutokana na ushiriki wa michuano ya kimataifa, uongozi wa Bodi ya Ligi umesema kuwa unasaka njia bora, ya kuhakikisha hakutakuwa na viporo vingi msimu huu.
Kwa sasa timu za Simba, Yanga, Azam FC na Singida Black Stars, zimeonekana kuwa na mechi chache zaidi za kucheza, ikilinganishwa na timu nyingine, kutokana na ushiriki wao wa kimataifa.

DAR ES SALAAM

Na Mwandishi wetu

Siku chache baada ya kutolewa katika michuano ya kimataifa, timu ya soka ya Singida Black Stars, imesema kuwa hasira zake itazimalizia katika mechi za ndani, ikiwemo Ligi Kuu Tanzania Bara.
Singida imekosa nafasi ya kutinga hatua ya robo fainali ya Shirikisho Afrika, baada ya kukusanya pointi ambazo haziwezi kumuweka katika nafasi mbili za juu.

Pwani

Na Mwandishi Wetu

Kuelekea katika mbio za Boston Marathon, zitakazofanyika nchini Marekani mwezi Aprili mwaka huu, Mwanariadha Staff Sajenti Alphonce Simbu, amewaomba wadau wa michezo kumsapoti gharama mbalimbali za ushiriki.
Mwanariadha huyo alisema kwamba, sasa anaelekeza nguvu zake zote kwenye maandalizi ya Boston Marathon, huku akiwa na kumbukumbu nzuri ya kumaliza nafasi ya pili mwaka jana.

MWANZA

Na Mwandishi wetu

Waziri Mkuu Dk. Mwigulu Nchemba amezitaka Wizara, Mamlaka za Serikali za Mitaa na Tawala za Mikoa, Taasisi na Mashirika ya Umma nchini, kuacha matumizi yasiyo ya lazima ili kuokoa fedha, zitakazoiwezesha Serikali kuendelea kutekeleza miradi ya maendeleo.
Dk. Mwigulu alitaja baadhi ya matumizi yasiyokuwa ya lazima, ikiwemo ununuzi wa magari mapya, wakati yaliyopo yanaweza kuendelea kutoa huduma, kuchapisha kalenda na kununua vifurushi vya zawadi.

ADDIS ABBA,

Ehiopia

Uaskofu Mkuu wa Ethiopia wa Emdibir, umeandaa kikao maalumu cha mafunzo kinacholenga ulinzi wa watoto, mpango unaotajwa kuwa ni muhimu ikizingatiwa kwamba, zaidi ya theluthi moja ya watoto nchini humo kwa sasa, wanakabiliwa na alama kubwa za udhaifu.
Programu hiyo iliundwa kwa ajili ya walimu wa vyama vya watoto katika Parokia mbalimbali, iliyofunguliwa na Mchungaji Abba Tesfa-Amlak Fikre, Mratibu wa Idara ya Uchungaji.

VATICAN CITY,Vatican

Mwadhama Pietro Kardinali Parolin, Katibu Mkuu wa Vatican, ametoa wito kwa Waamini kuona umuhimu wa umoja, kwani umoja katika Kanisa ni zawadi, na kwamba neema si upendeleo bali ni huduma.
Kardinali Parolin aliyasema hayo hivi karibuni, akiwa nchini Denmark kwa siku mbili, kama mjumbe wa Baba Mtakatifu Leo XIV, kwa ajili ya Maadhimisho ya Miaka 1200, ya kuanza kwa utume wa Mtakatifu Ansgar, ambapo alitumia nafasi hiyo pia kuwatia moyo Wakristo, kufanya mazoezi kila wanapopata nafasi

Na  Askofu Mstaafu Method Kilaini

Wahuni:    
Wahuni walikuwa wapiganaji wakali sana, na ndio walioleta matatizo yaliyozusha uvamizi. Wahuni walikuwa watu wa Mashariki ya mbali (Mongoliani, waasia wa ngozi ya njano). Wahuni walikuwa wachungaji wakiishi Kaskazini ya Milima ya Himalaya. 

Malisho yalipoisha, hawa wapanda farasi, walianza kuvamia nchi nyingine. Mwaka 200 Baada ya Kristo (BK), walikwea ukuta wakaivamia China na kusambaratisha himaya yake, na tangu hapo ikawa nyakati za giza kwa miaka 400 iliyofuata kwa China. 

MWANZA

Na Paul Mabuga

Mjadala wa “Uswahili ni nini”, uliibuliwa hivi karibuni na mchambuzi Maggid Mjengwa, akirejea fikra za Jenerali Twaha Ulimwengu na marehemu Edwin Mtei. 
Swali hili limezua taharuki chanya: Je, Mswahili ni nani katika ulimwengu wa leo? Je, bado ni yule “muongo muongo” aliyemchukiza Mtei, au ni utambulisho uliopata sura mpya, kuanzia mitaa ya Dar es Salaam hadi jijini Berlin?
Jenerali Ulimwengu, akizungumza hivi karibuni, katika makiwa ya marehemu Edwin Mtei, alifungua ukurasa wa kumbukumbu uliosisimua wengi. 
Alieleza kuwa Mzee Mtei alikuwa na msimamo usioyumba, dhidi ya kile alichokiita “Uswahili.” Katika muktadha wa kujiuzulu kwake Uwaziri, Mtei aliamini kuwa mfumo wa “Uswahili”, ulikuwa kikwazo kwa uadilifu wa kitaifa.

LONDON, Uingereza
Timu ya soka ya wanawake ya Jersey Bulls, imefanikiwa kuizaba Guildford Saints mabao 30-0, katika mechi ya Ligi ya Soka ya Wanawake ya Kaunti ya Kusini Mashariki mwa Uingereza, maarufu kama Surrey Division One.
Kwa ushindi huo wa maajabu, Bulls imekaribia kufikisha jumla ya mabao 100 ya kufunga, katika mechi zake 11 za Ligi ilizocheza.
Anita Tavares aliongoza kwa mabao tisa, ikiwa ni mara tatu zaidi ya Guildford, ambaye alifunga msimu mzima, huku wachezaji wengine 10 tofauti, wakipata bao katika mchezo huo.

DAR ES SALAAM

Na Arone Mpanduka

Panenka ni mbinu maalumu ya kupiga penati katika mpira wa miguu, ambapo mchezaji hupiga mpira kwa upole na kwa ustadi katikati ya lango, badala ya kupiga kwa nguvu kuelekea pembe za lango. 
Mbinu hii inalenga kumshawishi kipa kwenda upande mmoja, kabla ya mchezaji kupiga mpira polepole katikati, hivyo kumfanya kipa ashindwe kufikia mpira.